Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa kimataifa Mh. Bernard Membe aliyemuakilisha Rais Jakaya Kikwete katika Tamasha la Pasaka lililofanyika jana kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam jana. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama na katikati ni Naibu Waziri wa Sheria na Katiba Mh. Angela Kairuki.
Akizungumza na mamia ya mashabiki waliojitokeza katika tamasha hilo Mhe Membe amewaomba Watanzania kuwa watulivu wakati huu wa mchakato wa katiba mpya
Amesema uamuzi wa ni serikali gani iwe moja, Tatu au Mbili Wananchi ndiyo waaamua na wao wabunge watakipitisha kile kitachoamliwa na wananchi.
Mwanamuiki wa muziki wa injili kutoka nchini Afrika Kusini Keke Letse Phoofolo akicheza na mashabiki wake wakati alipokuwa akifanya vitu vyake kwenye uwanja wa Taifa jana.
Mwimbaji wa muziki wa injili kutoka nchini Zambia Ephraim Sekereti akiimba jukwaani jana. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...