Msemaji Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma, akizungumza wakati wa Semina maalum kwa 'Mablogger', iliyofanyika katika Hoteli ya Kilimanjaro Park, Misugusugu Kibaha, hivi karibuni. Semina hiyo imeandaliwa na Wizara ya Fedha kwa lengo la utaratibu wa kutimiza utekelezaji wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now).
*************************************************
Na Sufianimafoto Reporter
wizara ya fedha imeeleza wazi kuhusu mipango yake ya kutekeleza matokeo makubwa sasa(BRN) ikiwa ni utraatibu unaotumiwa na Serikali katika kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa baadhi ya majukumu yake kwa lengo la kupata matokeo makubwa kwa muda mfupi

Akieleza malengo hayo hayo msemaji mkuu wa wizara ya fedha, INGIAHEDI MDUMA amesema wizara ya fedha imejipanga Kutafuta mapato ya ziada kiasi cha shilingi trilioni 3.8 hadi kufikia mwaka 2015/16

Pamoja na hayo Mduma amesema pia wamedhamiria kupunguza nakisi katika bajeti ya Serikali kwa shilingi trilioni 4 kufikia mwaka 2015/16 na Kutekeleza miradi ya PPP yenye thamani ya shilingi trilioni 6 kufikia mwaka 2015/16

Malengo mengine ni kuhakikisha kwamba shughuli za BRN zinapatiwa fedha za kutekeleza miradi iliyopangwa ili kuweza kusimamia malengo yaliyokusudiwa 
Aidha amesema viashiria vya utafutaji wa mapato vinavyotekelezwa na Wizara ya Fedha vimegawanyika katika sehemu kuu nne ikiwemo ya mapato ya kodi, mapato yasiyo ya kodi, ubia katika sekta ya umma na sekta binafsi na kudhibiti matumizi ya serikali.

katika kuelezea malengo hayo amesema Katika kipindi cha Julai – Disemba, 2013 jumla ya shilingi bilioni 215.0 zimekusanywa kutokana na hatua mpya za kodi zilizoibuliwa kwenye maabara za BRN.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...