Afisa Muuguzi wa Hospitali Kuu ya Mnazimmoja Ashura Amour Mwinyi, akitoa maelezo kwa mgeni rasmi Mkurugenzi Mipango, Sera na Utafiti wa Wizara ya Afya Zanzibar Abdullatif Khatib Haji (alievaa shati jeupe), jinsi ya kuwasaidia watoto kupumua vizuri mara baada ya kuzaliwa. Hiyo ilikuwa hafla ya kukamilika kwa mradi wa kupunguza vifo vya wajawazito na watoto vitokanavyo na uzazi – MAISHA, unaofadhiliwa na Shirika la Misaada ya Maendeleo ya Kimataia la Marekani (USAID), katika ukumbi wa Hoteli ya Grand Palace Malindi.
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa kukamilisha mradi wa MAISHA kutoka mikoa yote ya Zanzibar wakimsikiliza Mkurugenzi wa mradi huo Dk. Dunstan Bishanga (hayupo pichani), akitoa hotuba katika mkutano huo.
Mkurugenzi wa Mradi wa kuboresha Afya ya mama na mtoto Tanzania Dk. Dunstan Bishanga, akitoa hotuba katika mkutano huo.
Mwakilishi wa USAID nchini Tanzania Lisa Patel, akitoa maelezo ya mradi wa MAISHA ambao umemaliza muda wake hapa nchini.
BOFYA HAPA KWA PICHA NA HABARI KAMILI
BOFYA HAPA KWA PICHA NA HABARI KAMILI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...