Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akifungua kikao cha kupitia taarifa ya Uandishi wa Ripoti za Kina (Thematic reports) zinazotokana na Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 kutoka kwa watalaam mbalimbali wa Wizara, Idara na Taasisi za Serikali kilichofanyika leo katika Hotel ya Peacock Jijini Dar es Salaam.
Mshauri mtaalam wa Sensa ya Watu na Makazi Bw. Collins Opiyo kutoka Shirika la Kimataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani akitoa ushauri wakati wa kikao cha kupitia taarifa ya ripoti hizo kilichofanyika leo katika hoteli ya Peacock jijini Dar es Salaam.
Wataalam wanaoandika Ripoti za Kina (Thematic reports) kutoka Wizara, Idara na Taasisi mbalimbali za Serikali wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa (hayupo pichani) wakati wa kikao cha kupitia taarifa ya ripoti hizo kilichofanyika leo katika hoteli ya Peacock jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 12, 2014

    Hizo ripoti zikionyesha matatizo tuliyonayo zinafanyiwa nini? Wizara na wilaya mbalimbali zinazifanyia kazi au zinasaidiaje maendeleo?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...