Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Injinia Mbogo Mfutakamba (katikati) wakati wa akizindua chapisho la Kanuni na utaratibu wa kuzingatia kwa Mamlaka zinazohusika na usimamizi na usambazaji wa maji nchini wakati wa mkutano wa mwaka wa wataalaam na watendaji wa usimamizi wa sekta ya maji nchini.
Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Injinia Mbogo Mfutakamba (katikati) akiwaonesha wataalam na watendaji wa usimamizi wa sekta ya maji nchini chapisho la Kanuni na utaratibu wa kuzingatia kwa Mamlaka zinazohusika na usimamizi na usambazaji wa maji nchini wakati wa mkutano wao wa mwaka jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Uwezeshaji wa Maendeleo ya Miradi ya Maji kutoka shirika la GIZ nchini Dkt. Fred Lerise akitoa ufafanuzi kwa wataalam wa maji kuhusu chapisho la Kanuni na utaratibu wa kuzingatia kwa Mamlaka zinazohusika na usimamizi na usambazaji wa maji nchini wakati wa mkutano huo wa mafunzo wa mwaka uliowahusisha wataalam na watendaji wa mamlaka za maji kutoka maeneo mbalimbali nchini.
Mtendaji wa Shirikisho la Wasambazaji wa Maji nchini (ATAWAS) Bi. Martha Kabuzya akizungumzia umuhimu wa chapisho hilo kwa sekta ya maji nchini na kutoa wito kwa mamlaka zote nchini kufanya kazi kwa kushirikiana ili kuhakikisha kuwa wateja wanaowahudumia wanapata huduma bora.
Sehemu ya Wataalam nawatendaji wa Mamlaka zinazohusika na usimamizi na usambazaji wa maji nchini waliohudhuria mkutano wa mwaka wa wataalaam na watendaji wa usimamizi wa sekta ya maji nchini.
Picha na Aron Msigwa - MAELEZO.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...