Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo mapema Machi mwaka huu alikabidhiwa nishani ya kumbukumbu ya Profesa M.O. Oyawoye aliyewahi kuwa Profesa wa kwanza duniani kutoka Bara la Afrika katika masuala ya jiolojia huko nchini Nigeria. Profesa Muhongo alikabidhiwa nishani hiyo na timu ya wanajiolojia kwa kutambua mchango wake mkubwa barani Afrika na duniani kwa ujumla. Nishani hiyo alikabidhiwa balozi wa Tanzania nchini Nigeria Mhe. Daniel Ole Njoolay kwa niaba yake.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akiwa ofisini kwake huku akiwa amevaa nishani hiyo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 10, 2014

    Well deserved prof!

    Mghaibuni

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 11, 2014

    Nishani hii na kazi zako ulizowahi kufanya zitakuwa na maana kama hutafanikiwa binafsi katika kazi yako ya sasa kama waziri wa nishati bali litafanikiwa taifa kwa mchango wako katika kuondoa tatizo la umeme na kuchangia watanzania kuhusishwa moja kwa moja kwenye umiliki na uzalishaji wa vitalu vya mafuta na gesi, vinginevyo hilo litabaki kuwa pambo binafsi.

    sesophy

    ReplyDelete
  3. Wanatutafuta hawa wanigeria wameanza na Raisi wetu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...