Watu zaidi ya kumi wamepoteza maisha kwenye ajali ya Daladala inayofanya safari zake kati ya Ubungo - Tegeta jijini Dar mchana huu,baada ya kushindwa maarifa ya kiudereva kwa Dereva wa daladala hilo hali iliyompelekea dereva huyo kuhama mpaka upande wa pili wa barabara na kulivaa lori kwa nyuma.Chanzo cha ajali hiyo inaelezwa kuwa ni mwendo kasi.
 Hili ndilo lori lililokuwa likipita katika upande huo wa Barabara na kufatwa na daladala hiyo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Emmanuel MganaJune 21, 2014

    Huyu dereva alikuwa anawahi wapi, amepoteza roho za watu bure, kama atakuwa hajafa basi sheria ichukue mkondo wake. Mungu azilaze mahali pema peponi Amiiinaaa. R I P wote.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 21, 2014

    Hicho kipande cha barabara kimewekewa alama za barabarani karibu kila baada ya mita 200.Maximum Speed ni 60Km.Kukiwa na foleni huwezi kugundua kama ni kipande hatari, lakini ni hatari.Speed rader (vitochi) vitumike au matuta yawekwe.Pole kwa familia ziliopotelewa na wapendwa nwaombea majeruhi wapone haraka.

    David V

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 21, 2014

    Innalillahi wa Inna ilayhi rajiun...Poleni wafiwa

    ReplyDelete
  4. polen sana ndugu zetu

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 21, 2014

    Habari za TV zinasema watu 6 ndio wamekufa na wengine 12 wamejeruhiwa

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 21, 2014

    jamani day waka watatimaliza!

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 21, 2014

    Bado speed limit. hawajaweka, madreva kuweni makini jamani

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 21, 2014

    Hizi ajali zime kuwa too much.Nadhani umefika wakati sheria za barabarani zipitiwe upya na kufanywa kuwa kali zaidi kwa wa kiukaji.Vilex2 jeshi letu la Polisi inabidi libadilike na kuacha kufanya kazi kwa mazoea lazima liende na wakati ili kuweza kukabiliana na wavunja sheria.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 21, 2014

    tatizo polisi wako bize na dili za kukakamata bodaboda na bajaji tu ,mambo ya kuangalia sheria za barabarani hayapo katika manifesto yao!!kwa hili hii ajali za kijinga kama hizi hazitapungua!!!
    Mdau mikocheni

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 21, 2014

    Jana ...wizi wa maafuta....juzi roli limevunja daraja...leo haya yanatokea.....bado nafikiria kurudi........R.I.P

    ReplyDelete
  11. Daaaaaaaah...mungu azlaze roho za marehmu mahali pemas peponi

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 21, 2014

    Too bad ila uzembe wa madereva kamwe abiria pia hawatakiwi kulifumbia macho suala la Ku overspeed.majina ya waliofariki na majeruhi yawekwe ili kusaidia utambuzi.RIP

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 22, 2014

    Mynz mungu awarehemu marehemu na kuwafanyia wepesi majeruhi,kaka hongera sana Kwa kuwasitiri victims wa Ajali Kwa kutotoa picha zao,mablogger wengine wajifunze kutoka Kwako

    ReplyDelete
  14. Madereva wengi wa siku hizi kwa kweli sijui wanajifunzia wapi udereva! wao ndio wamekuwa chanzo no1 kwa ajali za siku hizi. Hawana umakini kabisa. wamegeuza magari yamekuwa kama bodaboda. hawana umakini kabisa wanapoendesha.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...