Wadau tuwe makini wapi unapeleka kuosha gari lako. Vinginevyo utaishia kuoshewa wese lote kama hivyo...
Ankal. ​Kuna jamaa katoa maoni kuwa hatarudi Bongo baada ya kuona picha kwenye Globu ya Jamii ya  mtu kuiba wese kutoka kwenye gari. Ndugu kama huyo ni mmoja ya wanaopenda  sana kuiponda nchi yao  kama vile pote pengine ulimwenguni ni pepo. Ashakhum si Matusi Ankal, Rusha hii wapondaji  wakuu wa nchi yao (wajionee wenyewe hao wanaowaita wastaarabu  huku wakidai hawarudi Bongo) wakitia BIOFUEL kwenye tanki la mtu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 20, 2014

    Too bad
    hii tabia ya wizi imeota mizizi
    something has to be done

    ReplyDelete
    Replies
    1. Inabidi sasa tuwe makini maana hua wana eka maji

      Delete
  2. AnonymousJune 21, 2014

    Nafikiria sana kuhusu kurudi nyumbani.....kwakweli wenda nikajikataa mazima hukuhuku....

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 21, 2014

    Ama kweli kufiri ni mzigo kwa baadhi ya watu.Haiingii akili mtu kukana kwenu kwa kuogopa wizi!mbona hata Ulaya na USA wizi upo?

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 21, 2014

    Niko bongo baba/mama. Nachokoza tu

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 21, 2014

    Anonymous hapo juu wewe umeshaamua hurudi nyumbani, hapa ni unatafuta tu sababu za kuhalalisha kutokurudi kwako.
    Kuna sehemu rasmi za kusafisha magari, tutumie hizo, kwa kiasi ni salama. Pia funga gari wasafishe nje kwanza, wakisafisha ndani simama hapo uwaangalie, watu si waaminifu.

    ReplyDelete
  6. Mdau wa nne naunga mkono maoni yako. Hao wenye dhana hiyo ya kuogopa kurejea makwao ati kisa kuogopa matatizo au mambo kama hayo yatokeayo kila siku, mbona kote duniani yapo. Sana sana huwa tunatofautiana na mazingira na the way kila watu wanavyopractice maovu hayo, depends on the environments they're living in. Ila kote utapeli, wizi, ulaghai na vijitabia vyote hivyo vipo dunia nzima, hakuna muwaridi wowote ule na popote pale ulokosa kuwa na miba.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 21, 2014

    jamaa anashindwa kujielewa kuwa dunia inafanana tofauti ni rangi tu za watu ... lkn matendo yanafanana

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 21, 2014

    Hiyo inaitwa kupiga nyoka!!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 21, 2014

    Point well said mdau HK.Maovu yako kila mahali na kuna mengine yanatokea huko majuu na hayaja happen hapa nyumbani.ie kuna incidences nyingi za machizi kuingia kwenye Malls,movie theatres etc na kuua watu wasio na hatia kitu ambacho kwa hapa nyumbani so far ni unthinkable even though sio impossible.nini kuibiwa mafuta ya gari!!!

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 22, 2014

    Naomba kutofautiana na waliotoa maoni kwa kuzingata hiyo picha hapo.
    Hii picha sidhani kama ina ukweli; japo imefanya watu wachangie.
    'Huyo mtu anayeonekana kuweka hiyo BIO-FUEL kwenye gari ya mtu alipataje access wakati release handle ya fuel tank iko ndani? najua magari ya zamani unafunua tu kwa nje; ila mengi ni kwa funguo. Hii fotoshopu imeleta mtiririko wa maoni. Nawakilisha.
    Pia kusema hivyo sina maana tabia kama hizo hazipo; nina shaka tu na aliyetuma mada. Alitaka watu watoe maoni

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...