Kiungo wa Spain Cesc Fabregas (pichani) amefunguka leo kwa kusema alifanya
mazungumzo na kocha wa Arsenal Arsene Wenge kabla ya kuhamia Chelsea, na
kuambiwa kwamba nafasi yake tayari imeshacukuliwa na Mesut Ozil.
Fabregas alikuwa chagua la kwanza la Arsenal baada
ya mchezaji huyo alipoamua kuondoka Barcelona mwishoni mwa msimu uliopita,
lakini akamua kwenda Chelsea kwa dau la pauni milioni 30.
“Niliongea na Mzee Wenger naye akanambia atapata
wakati mgumu kumpa nafasi ya kucheza kwani tayari Ozil alikuwa ameshachukua
namba yangu”, Fabregas aliwaambia waandishi wa habari kwenye kambi ya Spain
huko Brazil.
“Kulikuwa na timu kadhaa ambazo ningeweza kuchagua
kwenda name nikachagua moja ya timu mbili ama tatu zilizo bora”, aliongezea
mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27.
“Nikaongea na Jose Mourinho naye akaongea mambo
niliyotaka kusikia na mambo yakaendelea haraka haraka kuanzia hapo.
“Huu si muda muafaka wa kuongelea hayo, hata hivyo,
kwani tunachohitaji ni kujali zaidi mambo ya timu ya taifa na kombe la dunia”,
alisema.
Fabregas aliingia kipindi cha pili wakati Spain
walipochapwa bao 5-1 na Holland katika mchezo wa kufungua dimba kwa kundi B.
Amesema yeye na wenzake wanatafuta hamasa kutoka mchezo wao na Uswisi miaka minne
iliyopita huko Afrika ya Kusini kwenye mechi ya ufunguzi.
“Tunahitaji kufikiria ni jinsi gani tuliweza
kuchuma katika miaka sita iliyopita,” alisema akimaanisha ushindi wa Spain
katika michuano ya Ulaya kati ya miaka 2008 na 2012.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...