Kituo cha uchunguzi na mafunzo ya magonjwa ya saratani, matumbo na ini Ukanda wa Afrika Mashariki kimefunguliwa rasmi mwishoni mwa juma. Sherehe hizo zilifanyika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili mwishoni mwa juma ambapo Mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal. Fuatilia katika picha matukio wakati wa ufunguzi.
Description: DSC_1474
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal akipongezana na Profesa Meinrad Classen wa Chama cha Madaktari wa Matibabu ya Mfumo wa Chakula ya Ujerumani ambaye alisaidia kutafuta fedha za kujenga na kuweka vifaa tiba vya kituo hicho kutoka Kampuni ua Else Kroner Fresenius ya nchini Ujerumani  baada ya kufungua rasmi kituo hicho.
Description: DSC_1477
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal
akisaini kitabu cha wageni mara tu baada ya kufungua kituo hicho.
Description: DSC_1482
Dkt. John Rwegasha, Bingwa wa Magonjwa ya Matumbo na Ini akitoa ufafanuzi kwa  Makamu wa Rais, Dkt. Bilal
Description: DSC_1501
Dkt. Edwin Masue Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani akitoa maelezo kwa Dkt. Bilal kuhusu matumizi ya kifaa cha kufanyia uchunguzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...