Kocha wa Uholanzi Louis van Gallakimpongeza Arjen Robben kwa kufanyiwa rafu iliyozaa penati na hatimaye bao la ushindi dhidi ya Mexico leo

Na Sultani Kipingo
wa Globu ya Jamii
Yaani huko Old Trafford katika  klabu ya Manchester United nchini Uingereza atakoenda kufundisha msimu ujao tayari waliishaanza kuandaa ofisi ya meneja wao mpya Louis van Gall anayeifundisha timu ya Uholanzi katika kombe la dunia, baada ya kuhisiwa kuwa ataaga mashindani hayo Jumapili hii walipocheza na Mexico. 
Unaambiwa hadi zikiwa zimesalia dakika tatu mchezo uishe, Uholanzi walikuwa bado wako nyuma kwa bao 1-0, huku kila mtu akiamini kuwa bao la kipimndi cha pili  la Mexico lillofungwa na Giovanni Dos Santos limewamaliza. 
Lakini baada ya kazi za ziada za kipa wa Mexico Guillermo Ochoa kuzuia Uholanzo wasilete madhara, Uholanzi ambao michuano iliyopita mwaka 2010 huko Afrika ya Kusini walifia fainali, wakapiga mabao mawili ya haraka haraka na kuwaacha Mexico hoi. 
Kwanza ilikuwa ni  Wesley Sneijder  aliyesawazisha mnamo dakika ya 87 kufuatia mpira wa kona uliomdondondokea akiwa katika mkao wa kula.
Ndipo katika dakika ya sita za muda wa nyongeza katika muda wa mapumziko mafupi ya kunywa maji, Arjen Robben aliangika chini baada ya kuchezewa rafu ndani ya 18. 
Wakati huo, tayari Robben alishakataliwa penati ya wazimkatika kipindi cha kwanza kilichotawaliwa na Mexico, na bila shaka safari hii alihisi anadaiwa kitu. Kwa vyovyote vile, Klaas Jan Huntelaar aliyeingia badala ya Robin van Persie ambaye ngoma leo ilimkataa, alifunga kwa mkwaju wa chini kuipa Uholanzi tiketi ya robo fainali.
 Dakika ya sita za muda wa nyongeza katika muda wa mapumziko mafupi ya kunywa maji Arjen Robben anafanyiwa madhambi
Wesley Sneijder  aliyesawazisha mnamo dakika ya 87 akifurahia

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...