Colombia imepeleka mashabiki wake wanaovutia kwa ushangiliaji wao hadi kwenye robo fainali za kombe la Dunia baada ya nyota wake James Rodriguez akifunga mabao yote. Colombia waliifunga Uruguay ya mng’ata meno Suarez bao 2-0 katika mchezo wao wa raundi ya 16 kweny uwanja wa Maracana jijini Rio de Janeiro jana.
Angalia goli la mwaka la Rodriguez ambalo ni tamu sana kiasi hata huchoki kuangalia. Huku goli la adui likiwa nyuma yake, kijana huyo mwenye umri wa miaka 22 kwanza aliweka gambani  pasi aliyoletewa, halafu kabla mpira haujatua ardhini aligeuka na kupiga bao dakika ya 28, akiwa nje ya 18.

Hebu cheki mwenyewe. Mambo kama haya ni marehemu Edward Chumilla tu aliyeweza kuyafanya hapa nyumbani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...