Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania – TRL unafuraha kuwataarifu  abiria wote na wananchi kwa jumla  kuwa kutokana na kukamilika ukarabati wa daraja eneo la bonde la mto Ruvu mkoani Pwani huduma ya treni ya abiria itaanza upya hapo siku ya Jumanne Juni 24, 2014 kutoka Stesheni ya Dar es Salaam saa 11 jioni. Wananchi wanotaka kusafiri wafike stesheni zilizo karibu yao kwa ajili ya kukata tiketi kuanzia  Juni 19, 2014.

Halikadhalika muda wa kuondoka treni kwa siku za Jumanne na Ijumaa kutoka Stesheni ya Dar kwenda Kigoma na Mwanza utakuwa saa 11 jioni na zile za kutoka Kigoma na Mwanza kuja Dar  katika siku za Alhamis na Jumapili ni saa 11 jioni  kutokea Kigoma na saa 12 magharibi kutokea Mwanza.
                                                                                         
 Tafadhali atakayesoma taarifa hii  amuarifu na mwenzake.
Uongozi wa TRL unawapongeza wananchi kwa ujumula kwa ushirikiano na uvumilivu waliouonesha wakati wakisubiri kukamilika kwa kazi ukarabati wa njia ya reli.

Imetolewa na Afisi ya Uhusiano ya TRL kwa Niaba ya
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji ,
Mhandisi  Elias Mshana
Dar es Salaam,

Juni 18, 2014.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...