Wiki hii jijini Dar es salaam kumefanyika Kongamano kubwa la wadau wa maji kutoka kila kona ya nchi hii. kubwa lililofanyiwa kazi na wataalam hao wa maji ni kujulishwa teknolojia mpya ya mabomba iliyokuwa inatambulishwa na kampuni kubwa ya teknolojia ya mambomba ya Borouge kutoka Falme za Kiarabu.
Borouge ilileta wataalam wanne ambao ni Mario Andrade, Farraj Tashman, Andrew Wedgner na Reda Ashkar. walionufaika na mafunzo hayo ni waliotoka Mamlaka za Maji mijini na vijiji, Wahandisi, Washauri katika fani zote za maji, ujenzi na gesi.
pia washiriki walifahamishwa kuwa sasa lile tatizo la mabomba ya matumizi yote yamefika mwisho kwani kiwanda cha pipe industries cha vingunguti mjini dar es salaam kitakidhi mahitaji ya nchi nzima na kuwa na ziada ya kuuza nje kwa amabomba ya aina zote kama vile hdpe, pvc, grp na mabomba chuma kwa upenyo wa 60mm mpaka zaidi ya 3,200mm.
Mgeni Rasmi katika kongamano hilo alikuwa Waziri wa Maji,Professor Jumanne Maghembe ambaye alionyeshwa kufurahishwa kwake na uwepo wa kiwanda kama hicho ambacho kinamilikiwa na wazawa kinahesabika kama kikubwa kuliko vyote afrika mashariki na kati pia cha aina yake kwa kuweza kuwa na uzalishaji wa mabomba aina yote katika kiwanda kimoja na chenye uwezo wa kuajiri watu 500.
Waziri wa Maji Professor Jumanne Maghembe (kulia) akikagua bidhaa za mabomba yanayozalishwa na kiwanda cha Pipe Industries cha mjini Dar es salaam wakati wa kongamano la wataaalam wa maji lilifanyika hivi karibuni. wa pili kushoto ni Mwekezaji Mzawa wa Kiwanda hicho Bwana Nassor Ally Seif.
Mwekezaji Mzawa wa Kiwanda cha Pipe Industries Bwana Nassor Seif (kushoto) akimsikiliza Waziri wa Maji Professor Jumanne Maghembe akimweleza jambo kuhusiana na mabomba yanayozalishwa na pipe industries wakati akikagua maonyesho ya kiwanda hicho katika kongamano la maji lilofanyika mjini dar es salaam.
Waziri Mageembe akizungumza na waandishi wa habari baaada ya kufungua kongamano la maji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...