![]() |
Mubelwa Bandio akimhoji Fabian Lwamba wa KRYSTAAL |
Katika NJE-NDANI wiki hii kati ya utakayosikia mahojiano na Fabian
Lwamba Mmoja wa ndugu watatu wanaounda kundi la KRYSTAAL ambao walizaliwa kwenye
familia iliyojiweza, lakini mgogoro wa kisiasa ukawafanya waikimbie Zaire
na kutengana.
![]() |
Michael, Fabian na Alistone Lwamba wanaounda kundi la KRYSTAAL |
Walikuja kuungana Canada ambako kwa miaka 16 wamekuwa pamoja kama kundi la
muziki wa injili
Wametoa albamu 6 na kupata tuzo 26
Pia utamsikia ripota wetu Sebastian Atilio ambaye amerejea kutoka safari ya
kupanda mlima Kilimanjaro.
![]() |
Sebastian Atilio na wenzake wakiwa kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro |
Aliona nini huko? Alijifunza nini? Ni kipi alichogundua kama udhaifu mkubwa
kwenye rasilimali zetu huko?
Yote haya na mengine mengi ni kwenye NJE-NDANI na Mubelwa Bandio, Jumamosi
kuanzia saa 6 kamili kwa saa za Marekani mashariki (NOON EST) kupitia
www.kwanzaproduction.com ama www.bordermediagroup.com
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...