Wafanyakazi wa kampuni ya Majembe Auction Mart wakifungua mashine ya kutengenezea matofali katika eneo la Kwa Msuguri, Kimara jijini Dar es Salaam.Wizara ya Maji iliamrisha kukamatwa kwa vifaa na mali mbalimbali za Martin Kessy aliyekuwa amejiunganishia maji kinyume na sheria na kufanya biashara ya kufyatua matofali.  Zoezi hilo linaendelea. Zoezi hilo limefanyika jana katika eneo la Kwa Msuguri, Kimara jijini Dar es Salaam jana.  .
 Mwenyekiti wa kamati maalum ya Wizara ya Maji, Eng. Hamis Blangson (kulia) akisikiliza jambo wakati wa operesheni maalum ya kupambana na watu wanaojiunganishia maji kinyume na sheria na kusababisha hasara kwa serikali na matatizo ya huduma hiyo kwa wananchi. Wengine ni wajumbe wa kamati hiyo, Bw. Twaha Mohamed (kushoto) na Bw. Juma Maingu (katikati).  Zoezi hilo linaendelea
Kifaa cha kubebea vifaa vizito cha DAWASA kikiondoka na moja ya mashine ya kutengenezea kutengenezea matofali katika eneo la Kwa Msuguri, Kimara jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 25, 2014

    The mdudu zee la kuona mbali,kwa mpangu huu ule mpango wa MATEKEO MAKUBWA SASA utafanya mambo yaende mswano kazeti buti maana mlilala mno ndio maana wanakuchezeeni kama vifaranga vya kuku.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 25, 2014

    Hebu waachieni watu wajiungie wenyewe mana mtu akitaka huduma atazungushwa wee mpaka atachoka

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 25, 2014

    Duhhh!

    Huu ni Uhandisi uliotukuka kwa mtu kuishia Darasa la Pili Shule ya Msingi halafu akajifungia mwenyewe mtambo wa kusukumia maji!

    Hapa ndio utaamini kuwa Watanzania huwa tunzazaliwa tukiwa tayari tumesha elimika!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 25, 2014

    Tungekuwa tuna utendaji wa namna hii kila idara Serikalini nadhani hata Raisi Jakaya Kikwete angalau na yeye angepumzika!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 25, 2014

    Au jamaa Kijogoo (aliye jiunganishia maji mwenyewe) aliwaruka Dwasco kuwapa chao?

    Nadhani ndio maana nao wakamzignua !!!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 25, 2014

    Ohhh, Tanzania imekuwa ni Italia ya pili?

    Kule ktk Italia maeneo ya Miji ya Kusini pana magenge ya Makundi ya Umafia yanamiliki kwa kuzishikilia huduma za maji na umeme kama idara za serikali!

    Haya mambo ya kudhibiti huduma za maji na umeme kwa makundi ya Kijambazi yapo Italia.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...