Gari likiwa limebeba mifuko yenye viuongo hivyo, ambapo Jeshi la Polisi wilaya ya Kinondoni limesema kuwa limeanza uchunguzi wa kina baada ya kukakamata viungo mbalimbali vinavyodhaniwa kuwa ni vya binadamu katika  mifuko ya plastiki katika machimbo ya kokoto sehemu za Mbweni Mpiji, Magohe, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam. 
Habari zinasema  kwamba  hayo ni masalia ya viungo vya binadamu vilivyotupwa maeneo ya kutoka  chuo kimoja cha udaktari (jina kapuni kwa sasa)  baada ya wanafunzi kumaliza kutumia kwa mazoezi. Viungo hivi vilitupwa baada ya kukosa pesa za kuteketeza kwenye tanuri maalum. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kanda Maalumu ya Dar es salaam Suleiman Kova anatarajiwa kuzungumza mchana huu juu ya sakata hilo.
 Sehemu ya mifuko ya plastiki iliyokutwa na viungo hivyo ambavyo inasemekana ni pamoja na mikono, miguu, ngozi na sehemu nyingine za miili

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 46 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 21, 2014

    Jamani jamani jamani!!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 21, 2014

    Dalili za kiyama hizo leo tumefika hapo tunaona kila jambo baya ktk macho yetu kila aina ya zambi kubwa kubwa zinafanywa bila kisisi kwa zambi ambazo tunazofanya naweza kusema hata kabla yetu hawakuwahi kufanya inasikitisha sana

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 21, 2014

    Kiukweli dunia imeisha ... Unyama umetawala yani dah!!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 21, 2014

    Eeeeh Mungu ni wapi tuelekeako taifa hili!watu hawana hata chembe ya huruma!nahisi kulia na kuzzimia,Mungu tusaidie

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 21, 2014

    Kweli ukistaajabu ya Musa....

    ReplyDelete
  6. Uuuwi maiti zote hizo zimetoka wapi? Naogopa mie

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 22, 2014

    The mdudu,ndugu zangu watanzania kwakweli nchi ilipofikia ni pabaya sn tena sn mauwaji kama haya enzi ya mwalimu nyerere utaanzia wapi? Yaani siku hizi mtu akipotea yaani kuanzia ndugu hadi mjumbe wa nyumba kumi hawajui? Hii ni hatari sn na ni janga la taifa,tukumbushane enzi za mwalimu kipindi kile mikusanyiko ya vijana kupiga domo la siasa ilikua marufuku na ilitusaidia sn kuondokana na jaziba za wanaadamu wasio na utu kwawezao lakini leo hii vijana wakiwa kwenye mikusanyiko baada ya pilika za mchana basi kinachofuata ni siasa kwenda mbele matokeo yake ndio haya tunayoyaona leo hii mtu anaongea siasa na jaziba juu mpaka povu linamtoka mdomoni akitoka hapo anaanza kumvizia mpinzani wake na kummaliza utasema yeye ndie aliemleta hapa duniani,,ndugu zanguni chonde chonde tubadilikeni tunalitia aibu taifa letu na chakushangaza watu haohao waliohusika wakitiwa mikononi mwa serikali kunatokea watu wanaojiita wanasheria nakuanza kuwatetea huu ni ujinga na upumbavu watu kama hao wakitiwa nguvuni ni kunyongwa au maisha jera,huku kuteteana kijingajinga ndio maana watu hawachoki au kuogopa kufanya kitu mbaya coz wanajiamini kuna watu watawatetea,,nimechefuka kweri moyoni kuona tunauwana kama wanyama

    ReplyDelete
  8. Mmmh hadi tumbo linauma inatisha kwa kweli

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 22, 2014

    hii inaonyesha ni jinsi gani watu wanavyojali pesa kuliko utu na yote hii ni kwa sababu ya tofauti kubwa za kipato miongoni mwetu, kukamata na kuwaadabisha hawa ni njia moja wapo ya kudhibiti matukio kama haya lkn pia suluhu ya kudumu ni kutatua matatizo ya kiuchumi na kijamii tulionayo, ikiwemo pamoja na kugawanya rasilimali za taifa ktk uwiano unaolingana na kupambana na mmomonyoko wa maadili kwa kujenge tabia na utamaduni wa kujipatia kipato kwa njia halali na za haki,
    this is too bad

    ReplyDelete
  10. ArifbiyaoJuly 22, 2014

    Kwanini tanzania tusiwe na sheria kama china tunadumisha urafiki na china lakini hatufuati nyendo zao hao ni wakunyongwa tu na tena wakatwe katwe na wao ili iwe fundisho kwa wengine watakaofikria kufanya unyama kama huu aisee inaumaa sanaaa

    ReplyDelete
  11. Watanzania bwana....hivyo vimetumiwa na wanafunzi wanaosomea udaktari bila shaka..cjui kwann wamevetupa ovyo namna hiyo

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 22, 2014

    Mamboa kama haya yalikuwa na nguvu sana India na China na nchi nyingine za Asia mabako watu uvuna viungo kwa ajili ya kuuza (tansplant) kwa wagonjwa matajili: Mradi huu lazima kuna hospitali, madaktari na wenye ujuzi wa kuvuna viungo na kuvitunza vizuri, na pia kusafisha nje ya nchi: Fanya utafiti utaona kuwa ni mpango mzito "Mafia"

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 22, 2014

    Gari ni la nani?
    Nambari za usajili?
    Dereva ni nani?

    Yaani hakuna mtu aliyeweza kunusa hiyo harufu mbaya?

    Vipande hivyo vilinyunyizwa dawa visioze au kutoa harufu mbaya?

    Je, ni ushirikina?

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 22, 2014

    Innallilahi waina ilahi rajiun! SubuhanaAllah wapi tunakoelekea wanaAdam hapo ndio Tunajiuliza security ya nchi ipo wapi? Kuanza uchunguzi mkubwa watu watangaze watu wao wanampotea DNA zifanye kazi hii Inatisha ndani ya nchi na Border kuwe na uchunguzi mkubwa na usalama wa Ulinzi. MZ

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 22, 2014

    Viungo vilikuwa vikitumiwa kama practical kwa wanafunzi wa udaktari.
    Acheni kucheemka

    ReplyDelete
    Replies
    1. AnonymousJuly 22, 2014

      Wahisi nani amechemka hapa?Hata kama miili hii ilitumika kama practical kwa wanafunzi maana ya utupwaji huo wa wazi kama mizoga ya Kunguru maana yake nini?Udhalilishaji wa binadamu haukubaliki kokote duniani labda Kichwani kwako tuu

      Delete
  16. Mungu tusaidie.

    ReplyDelete
  17. AnonymousJuly 22, 2014

    Is this not medical waste?

    ReplyDelete
  18. AnonymousJuly 22, 2014

    Unaweza ukazimia kwakweli

    ReplyDelete
  19. AnonymousJuly 22, 2014

    Kweli, mwacheni Mungu aitwe Mungu. Kweli ee kweli ee, Loo! nimegundua kwa nini watu wanakimbia Tanzania sasa kwa mtindo huu nyumbani hakufai loo! Ee Mola tuepushe

    ReplyDelete
  20. AnonymousJuly 22, 2014

    Haya sasa nyie mnaojiita ma doctor tupeni forensic mtuambie hao ni wa kina nanii? Au mtuambie bac wanawake ni wangapii na wanaume pia ndo tutajua kweliii bongo tuna ma doctor au wote mburulaz? Pia tunataka nyie viongoz wekeni tip line ili watu wajitokeze wawataje hao wahusika sio tuuu blah blah nyingiii zisizo na mafanikioo, fanyeni kazi mnaitia aibu nchi yetu Tanzania! !!!

    ReplyDelete
  21. AnonymousJuly 22, 2014

    Hii yote inatokana na kutokuwa na viongoz waadilifuuu, n chi yetu haina viongoz shupavu swala kama hili wangechukua hatua za haraka kwa kaweka tip line kama Kuna mtu anajua mtu aliyefanya hivyo ajitokeze, ndo marekani huwa inafanya hivyo ili kupata muhusika kwa haraka, waweke dau la million 5 au 10 wa one kama hawato mpata muhusikaa, na sio blah blah nyingiii bila kutatua tatizo haisaidiiiii

    ReplyDelete
  22. AnonymousJuly 22, 2014

    Naona kuna na vifaa vingi vinavyotumika hospitalini (gloves) jambo linalonifanya niamini kuwa viungo hivyo vimetokea kataika moja ya hospitali kubwa hapa jijini. Huenda vinatokana na wagojwa kukatwa viungo hivyo kutokana na matatizo mbalimbali kama kusukari na mengineyo. Ila kwa nini wameamua kuvitupa kwa namna hiyo hilo ndio swala la kujiuliza.

    ReplyDelete
  23. AnonymousJuly 22, 2014

    Mwenyezi mungu naomba utusaidie Tanzania.

    Kwanza kabisa, nimejiuiza sana, nahisi kuna mambo MATATU. 1). INAWEZEKANA HIVI VIUNGO VILIKUWA VINATUMIKA KATIKA MAZOEZI KWA VITENDO KWA MADAKTARI WETU, KAMA NI KWELI KWANINI WASIVIFADHI KATIKA UTARATIBU UNAOKUBALIKA KISHERIA! KAMA JIBU NI DIO BASI SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE KWA KUSHINDWA KUTUMIA NJIA SAHIHI YA KUVITEKETEZA NA KUSABABISHA HOFU KWA WANANCHI.

    2). KAMA KAMA LA, NI KWA VIPI WALIWEZA KUPATA VIUNGO VYA BINADAMU WENGI KIASI HIKI, NI KWA WATU WALIOPOTEA AMA KWA KUUWAWA JAMANI MBONA INATISHA SANA!

    AMA USHIRIKINA? TUNAOMBA HUYO DEREVA ASEME ALIVITOA WAPI NA KAMA BADO KUNA VIUNGO VINGINE VIMEBAKIA HUKO ALIKOVITOA ALEZE KILA KITU ILI SHERIA IFUATE MKONDO WAKE.

    MUNGU BABA TUNAOMBA UOKOE TAIFA LA TANZANIA.

    ReplyDelete
  24. AnonymousJuly 22, 2014

    mimi mwenzenu kwa miaka mingi nimekuwa najiuliza bila kupata jibu, nikiangalia luninga, ITV-Jiji letu, mara kwa mara unakuta tangazo la watu walio potea, kwa mwenzi ukifuatilia ni watu wengi, cha kushangaza sioni kama kuna mtu anae ona uzito wa hili swala,wanapotea wanaenda wapi? je huwa wanapatikanaga? na kwa nini watu wengi hivyo wanapotea, maana wiki haiishi lazima kuna mtu anatangazwa kapotea. Yani hadi naogopa, sasa hii ya leo ndio kali kuliko. Watanzania tunasubiri majibu tena yanayo jitosheleza.

    ReplyDelete
  25. AnonymousJuly 22, 2014

    Hiyo hadi Gloves kuwepo itakuwa inatoka Hospital...Lkn hatakama ni hospital kwanini waende wakatupe Dampo? Je mtoto au binadamu uliye hai ukiona hivyo, wanatujengea nini? Watoto wetu wanawajengea nini? Si ndio watatuzoesha kuona maiti na watoto wetu wataona kama maiti na kuua ni kitu cha kawaida...

    Kwani hiyo imekuwa kuku atupwe jalalani...? Kwanini wasizike? Mbuzi mwenyewe au ng'ombe akifa hatupwi jalalani sembuse viungo vya binadamu!! Jamani kama ni Hospitali kwa hakika sheria ifuate mkondo...

    ReplyDelete
  26. AnonymousJuly 22, 2014

    Tunajua fika kuwa Mahospitali kama Muhimbili huwa wakati mwingien wanatumia Maiti zilizokuwa na wenyewe kujifundishia kwa Madoctor. ila kwanini watupe masalia Jalalani kama wanatupa taka za kawaida?

    Si vizuri kabisaa...Wangezika basi kama wameshindwa kuchoma.

    ReplyDelete
  27. AnonymousJuly 22, 2014

    Tunaelekea wapi sasa maana huku tulipofika sipo ambapo tulitarajia na haya yote husababishwa na sisi wenyewe kwakweli inatisha sana imefikia wakati tutaogopa hata kwenda kwenye nyumba za ibada kuhofia maisha yetu

    ReplyDelete
  28. AnonymousJuly 22, 2014

    " YARABI TOBA "

    ReplyDelete
  29. Kiukweli ni hatari sana mie sina la kusema

    ReplyDelete
  30. AnonymousJuly 22, 2014

    Inasikitisha sana, tuwe watulivu tusubiri kupata ukiweli wa hizi maiti kutoka kwa serikali

    ReplyDelete
  31. AnonymousJuly 22, 2014

    CADAVA.....Hizi ni sampuli za maiti kwa ajili ya kujifunzia madaktari jamani...acheni kukuza mambo namna hii....kosa la chuo hicho ni kudspose vibaya...walitakiwa kuchoma maiti hizi.

    By KAFANABO/MNYAKYUSA PURE/DR

    ReplyDelete
  32. AnonymousJuly 22, 2014

    subhannallah

    ReplyDelete
  33. AnonymousJuly 22, 2014

    hivi mi nahisi wanauza nyama ya watu

    ReplyDelete
  34. AnonymousJuly 22, 2014

    inavosemekana waliitupa baada ya kuona wakaguzi wanakuja but the issue is why waliogopa hadi wafike stage ya kutupa ovyo,...and why kama ni halali kutumia viungo hivyo kwa kufanyia practicals zao na kama ni legal waogope hadi kufanya hivi.....

    ReplyDelete
  35. AnonymousJuly 22, 2014

    Ndio madaktari wanafunzi hutumia miili/maiti kujifunza umbo (anatomy) la mwili wa binadamu. Lakini baada ya kumaliza kuitumia miili, huchomwa kwa utaratibu maalum. Na wala watu wa nje (wasio katika fani) hawasitahili kilijua hili. Miili ya binadamu inastahili kuheshimiwa siku zote. Hicho ndicho nilichoambiwa na profesa wangu siku ya kwanza kabisa ya somo la anatomy. Huwezi kwenda kutupa mabaki ya mwili wa binadamu kwenye dampo. Inaonekana hivi vyuo vingine ni vyuo uchwara. Kama viongozi wake wanaweza kufanya hivyo, je ni aina gani ya madaktari wanazalisha? Maadili yako wapi? Sheria ichukuwe mkondo wake.

    ReplyDelete
  36. AnonymousJuly 22, 2014

    These families donated their bodies to make us better doctors! I remember my cadaver like it was yesterday (trained 15 years ago)... I hold so much respect for her. I even wrote a poem at our last gathering ya kuwapa familia majivu take.... How could this institution be so inhuman... sasa hiko chuo kifutwe kabisa au walipe fidia yakutosha sio kwenda conference na kula padiem tu eti hawana pesa za kuchoma disgusting!

    ReplyDelete
  37. AnonymousJuly 22, 2014

    Du! Hii ni hari! Kwani hizo practical zipo mwaka huu tu?!! Hasbunaalah wa neema llwaakiiil.

    ReplyDelete
  38. AnonymousJuly 22, 2014

    Duuh,hii hatari kubwa sana,ubinaadamu upo wapi jamani? Nawaza sana!!!!!!!!!!!!!

    ReplyDelete
  39. AnonymousJuly 22, 2014

    Ubinaadamu upo wapi jamani? Watanzania wapi tunaenda? Nawaza saanaa!!!!!!!!!

    ReplyDelete
  40. AnonymousJuly 22, 2014

    Hakika sheria ifuatwe na wahusika wakamatwe haijalishishi walitumia kwa mazoez au la!

    ReplyDelete
  41. AnonymousJuly 22, 2014

    Yaaani. Eeee. Roho ya binadamu hao imekuwa ngumu hivi ? Wanasahau kuwa hicho kilikuwa sehemu ya mtu, pengine wengine wapo hai ? Na je we mhusika au wahusika ungefurahia kufanyiwa hiki kitendo ? Je ingekuwa ni kiungo cha familia yako ungesema haikugusi ? Wapi dhamira ? Na sasa sisi tuna simama na kusema mumefanya makosa. Hata madaktari wana ethical conduct ya ku dispose off viungo na mengineo. Hii inatuletea aibu kubwa sana kwenye jamii ya Afrika. Mbona mnaturudisha nyuma kimaadili hivi ? Nyie wachache kweli mumetuvunjia heshima kabisa. Mnatakiwa mujitokeze na mkiri mmekosa. Hiyo ni adhabu tosha. Naomba msibanie hii comment. Lazima wakuu wa idhara hii mtoe commentary, nyie mkinyamaza kimya tutayaona tena haya, ni aibu.
    Mungu upo wapi ? Amani imeshaondoka nchini, tamaa, ufisadi, ushirikana, ndiyo unatawala. Na ni wachache wanakosa hii nidhamu. Tusaidie Mungu.

    ReplyDelete
  42. Ni kweli inasikitisha kwani sio mazoe yetu watanzania kuona viungo vya binadamu hadharani kiasi hiki tena vikiwa vimetupwa jalalani. Lakini basi niseme nini nijuacho; Mimi nawalaumu sana wahusika waliamua kutupa viungo hivi vya binadamu katika hali hiyo, nijuavyo hawa ni Madaktari wetu wanafunzi ambao utumia miili ya binadamu katika moja ya masomo yao, na miili hiyo uipata ni katika zile maiti zisizo na wenyewe ambazo hukaa machuari kwa muda mrefu bila kupata ndugu zao, na hivyo ndizo zinazotumika katika kujifunza kwa Madaktari wetu.
    Sasa utaratibu ambao wameutumia hawa Menejimenti ya Hospitali (I......) ambapo si Madaktari tena kwenda kutupa kwa styre hile sio mzuri nadhani pamoja na kumaliza kuitumia miili hiyo walitakiwa kuchimba shimo kubwa na kufukia viungo hivyo na tena kwa kupata kibali cha Police ili kuepukana na lawama kama hizi ambazo zimesonga akili za watu pasi sababu yeyote wakati watu wanawaza nini leo wafanye katika maisha yao kisha wanakutana na habari hizi za kustua, hakika Uongozi wa Hospitali hiyo ya (I......) haikufanya vizuri.
    Ikumbukwe Binadamu ni Binadamu tu haijalishi kafa kifo gani au alikuwa na tabia gani Maiti yake yapaswa kuheshimiwa! Hawa uongozi(Taifa lao) wanatudharau sana sisi waafrika, hivyo wachukuliwe hatua stahiki pux&*o#@)* hawa!

    ReplyDelete
  43. AnonymousJuly 24, 2014

    Mimi ni Mwanafunzi wa udaktari na ninakiri uwepo wa hizo practical vyuoni lakin nimesikitishwa sana na kitendo kilichofanywa na huo hicho..Ni wazi kwamba mtu hutokuwa daktari bila kujifunza pratical hizo mwaka wa kwanza,Lakin kuna maadili yanayotuongoza na mwili wa binadamu unatakiwa uheshimiwe...sidhana hata huyo mtupaji angependa ndugu yake atupwe kwa staili ile...hata kama hawana pesa basi wangewazika kwapamoja.....Hicho huo kipo after money na wahindi hawajaithamin miili kwa sababu ni ya watu weusi....CHUO KIWAJIBISHWE maana practical hizo ni siri mtu yeyote asiyehusika hastail kujua...

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...