Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni ya ufuaji umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) Bw. Harbinder Singh Sethi (wa pili kulia) akimwonyesha kitu Fadha Gerald Kamina (wa pili kushoto) mara baada ya kukabidhi hundi ya Shilingi milioni 14.5 kama msaada kwa jumuiya ya Kanisa la Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam, kusaidia ujenzi wa kanisa hilo. Kushoto ni Bi. Rose Rupia, Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa Kanisa hilo na kulia ni Rajiv Bhesania, msaidizi wa Mwenyekiti mtendaji wa IPTL.
 Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni ya ufuaji umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) Bw. Harbinder Singh Sethi (wa pili kulia) akikabidhi hundi ya shilingi milioni 14.5 kwa Fadha Gerald Kamina (wa tatu kilia), kama msaada kwa jumuiya ya Kanisa la Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam, kusaidia ujenzi wa kanisa hilo. Pamoja nao ni Bi. Rose Rupia, Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa Kanisa hilo (wa tatu kushoto), Katibu na Mwanasheria Mkuu wa IPTL Bw. Joseph Makandege (wa pili kushoto), Mwanasheria wa IPTL Melchisedeck Lutema (wa kwanza kushoto) na wa kwanza kulia ni Rajiv Bhesania, msaidizi wa Mwenyekiti mtendaji wa IPTL.
Katibu na Mwanasheria Mkuu wa IPTL Bw. Joseph Makandege (wa pili kushoto),  akimpongeza Fadha Gerald Kamina (wa tatu kilia), mara baada ya Mwenyekiti Mtendaji wa IPTL Bw. Harbinder Singh Sethi (wa pili kulia) kukabidhi hundi ya shilingi milioni 14.5 kama msaada kwa jumuiya ya Kanisa la Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam, kusaidia ujenzi wa kanisa hilo. Pamoja nao ni Bi. Rose Rupia, Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa Kanisa hilo (wa tatu  kushoto), Mwanasheria wa IPTL Melchisedeck Lutema (wa kwanza kushoto) na wa kwanza kulia ni Rajiv Bhesania, msaidizi wa Mwenyekiti mtendaji wa IPTL.

=========   ======  =======   =====


KAMPUNI ya ufuaji umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) imetoa msaada wa shilingi milioni 14.5 kwa jumuiya ya Kanisa la Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kusaidia ujenzi wa kanisa hilo.


Akizungumza katika hafla ya kukabidhi hundi kwa jumuiya hiyo, Mwenyekiti Mtendaji wa IPTL, Bw. Harbinder Singh Sethi alisema kuwa IPTL imetoa msaada huo ili kusaidia katika ujenzi wa Kanisa hiyo ya Mtakatifu Petro.   


“Hizi milioni 14.5 tulizotoa kwa Kanisa la Mtakatifu Petro, ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wetu wa kuwezesha miradi mbali mbali za kijamii ambazo zinagusa maisha ya watu wengi. Tuna imani kwamba kwa kuchangia fedha hizi zitasaidia kusukuma mbele ujenzi wa kanisa hili ili liweze kukamilika mapema na kutumika kwa ajili ya ibada. 


“Jitihada hizi ni moja kati ya mkakati wetu wa utekelezaji wa mpango wetu wa kutumia sehemu ya faida tunayopata kutokana na shuguli zetu, kwa kuiwezesha jamii katika nyanja mbali mbali za kimaendeleo ikiwemo kiuchumi. Misaada kama haya hayalengi tu kusaidia vijana wa kitanzania kuendelea kiuchumi lakini pia misaada kwa taasisi za kidini itasaidia katika kujenga jamii inayo mcha Mungu na hivyo taifa kuwa katika mazingia mazuri ya kupiga hatua kubwa kimaendeleo,” alisema Sethi. 


Bw. Sethi alisema kuwa kampuni yake ina mpango madhubuti unaolenga kusaidia mashule, makanisa, misikiti na mashirika mengine yasiyoyakibiashara yanayofanyakazi ili kuwawezesha vijana kuwa wachangiaji wakubwa kwenye maendeleo ya kiuchumi Tanzania. 


Naye Katibu na Mshauri Mkuu wa IPTL, Bw. Joseph Makandege alisema kuwa IPTL ikiwa na mpango wake wa kuunga mkono jitihada mbali mbali za kimaendeleo na kijamii, itaendelea kushirikiana na jumuiya mbali mbali ili kwa pamoja kuona kwamba fursa mbali mbali za kiuchumi zinazojitokeza zinapewa msukumo kwa ajili ya maendeleo ya jamii kwa ujumla. 


“Kama IPTL, tumeona kuwa ni jukumu letu kuisaidia jamii inayotuzunguka. Nina imani mchango wetu kwa Jumuiya ya Mtakatifu Petro leo hii utasaidia kuongezea nguvu ujenzi wa Kanisa unaoendelea. Lengo letu ni kuona kwamba tunachangia maendeleo ya kiuchumi lakini pia bila kusahau jamii yetu inayotuzunguka zikiwepo jumuiya mbali mbali za kidini,” alisema Bw. Makandege.  


Kwa upande wake, Bi. Rose Rupia, Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa Kanisa hilo, aliishukuru IPTL kwa msaada wake na kusema kuwa fedha iliyotolewa itasaidia kwa kiasi kikubwa kusukuma mbele ujenzi wa kanisa hilo ambao bajeti yake ni zaidi ya shilingi milioni 600. 


“Naishukuru IPTL kwa kuona umuhimu wa kukubali ombi letu na kuja kutuunga mkono katika jitihada za ujenzi wa kanisa letu. Fedha hizi zitasaidia kusukuma mbele zaidi ujenzi wa kanisa letu, huu ni mfano mzuri wa kuigwa na makampuni mengine na watu binafsi,” alisema Bi. Rupia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...