Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe Jordan Rugimbana leo amezindua rasmi utoaji wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi Wilaya ya Kinondoni, na kuwa mtu wa kwanza kupokea kitambulisho chake mbali na kuwakabidhi wananchi 22 Vitambulisho vyao kutoka Kata ya Saranga mtaa wa Matangini.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Rugimbana akikabidhiwa
Kitambulisho chake na Afisa Usajili Wilaya ya Kinondoni Ndugu Abdulrahman Muya
baada ya kukamilisha hatua za mwisho za
uhakiki leo Kata ya Saranga Mbezi Dar-es-salaam. Kushoto ni Bw. Dickson Mbanga
Weiss Afisa Usajili Kinondoni
Mmoja
wa wananchi wa Kata ya Saranga akiongozwa na Afisa Usajili wa NIDA kukamilisha hatua za mwisho za kuhakiki taarifa zake
kabla ya kukabidhiwa kitambulisho chake leo, Kata ya Saranga Mbezi
Hapa anamkabidhi mmoja wa wananchi Bi. Chiku Issa
Waziri kitambulisho cha Taifa, akishuhudiwa na Maafisa Usajili katika
Wilaya Bw. Dickson Mbanga Weiss na Bw.
Abdulrahman Muya
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...