Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimlaki Mwana Mfalme wa Japan Prince Akishino alieambatana na Mkewe Princess Akishino walipomtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo July 3, 2014.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha Mkurugenzi wa Idara ya Asia Bw. Mbelwa Kairuki kwa Mwana Mfalme wa Japan Prince Akishino na Mkewe Princess Akishino waliomtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo July 3, 2014.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazunzumzo na Mwana Mfalme wa Japan Prince Akishino na Mkewe Princess Akishino Ikulu jijini Dar es salaam leo July 3, 2014. walioketi kulia ni Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe akifuatiwa na Balozi wa Tanzaia nchini Japan Mhe Salome Sijaona
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwapa historia ya Ikulu Mwana Mfalme wa Japan Prince Akishino na Mkewe Princess Akishino mbele ya lango kuu ya Ikulu hiyo ya Dar es salaam.
|
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwatembeza Ikulu Mwana Mfalme wa Japan Prince Akishino na Mkewe Princess Akishino jijini Dar es salaam leo July 3, 2014.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mwana Mfalme wa Japan Prince Akishino na Mkewe Princess Akishino walipomtembelea jijini Dar es salaam leo July 3, 2014. Wengine ni WaZiri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe (wa pili kulia) ,
Naibu WaZiri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Dkt Mahadhi Juma Maalim, balozi wa Tanzania nchini japan Mhe Salome Sijaona (kushoto) na balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe Masaki Okada (wa pili kushoto).
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwaonesha Simba waliotengenezwa Mwana Mfalme wa Japan Prince Akishino na Mkewe Princess Akishino walipomtembelea jijini Dar es salaam leo July 3, 2014.
3 Julai, 2014
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete asubuhi ya
leo, Alhamisi, Julai 3, 2014, amemkaribisha Ikulu, Dar Es Salaam, Mwana wa
Mfalme wa Japan, Prince Akishino pamoja na mkewe Princess Akishino.
Mwana
Mfamle huyo ambaye anatembelea Tanzania, amewasili Ikulu kiasi cha saa nne
asubuhi na kufanya mazungumzo ya zaidi ya nusu saa na Mheshimiwa Rais Kikwete.
Katika
mazungumzo yao, Rais Kikwete amesema kuwa Japan ni mshirika mkubwa na muhimu
sana wa maendeleo ya Tanzania. “Tunathamini sana mchango wenu katika
maendeleo ya Tanzania na tunaendelea kuwashukuru sana. Ukizunguka nchini mwetu
utaona kwa macho yako miradi mingi na mikubwa ambayo imejengwa ama inajengwa kwa
msaada wa Japan.”
Rais
kikwete ameongeza: “Pamoja na ushirikiano huu. Bado tunaamini kuwa Japan inaweza kusaidia
zaidi Tanzania hasa kwa kushawishi makampuni yake kuwekeza katika sekta
binafsi. Ukipita mitaa ya Dar es Salaam, magari tisa kati ya 10 ni ya Kijapan.
Ukiingia katika maduka ya vyombo vya elektroniki - televisheni, kompyuta, camera, karibu kila
kitu kinatoka Japan. Hali hii inathibitisha kuwa bidhaa vya Japan zina soko
kubwa na zinaweza kuzalishwa hata hapa nchini na makampuni binafsi.”
Rais
Kikwete pia ameitaka Japan kuangalia jinsi gani inavyoweza kusaidia ongezeko la
watalii kutoka Japan kuja kutembelea Tanzania kwa kuanzisha safari za ndege za
moja kwa moja kutoka huko hadi Tanzania na nchi nyingine za Afrika.
“Wataalii
wengi kutoka Japan wanashindwa kuja Afrika kwa sababu hakuna shirika hata moja
la ndege la Japan ambalo lina safari za kuja Afrika, hata Afrika Kusini hakuna.
Hii ndiyo maana hatuoni watalii wengine kutoka nchi za kusini mashariki mwa
Bara la Asia kutembelea vivutio vyetu vya utalii,”
amesema Rais Kikwete na kuongeza:
“Kama
kuna jambo halionekani sasa katika uhusiano wa Tanzania na Japan ni uwekezaji
katika sekta binafsi. Hili ndilo jambo tunaloliomba.”
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU
DAR ES SALAAM
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...