Ndugu Wanajumuiya,

Mkutano wa Wanajumuiya wote utafanyika Jumamosi, tarehe 2 Agosti 2014 kwenye Jengo la Ubalozi address hii: 30 Overhill Rd, Mount Vernon, NY 10552 (Pale pale tulipofanyia uchaguzi mwaka jana, 2013), kuanzia saa nane mchana hadi saa moja jioni. 

Mkutano utajadili maendeleo ya Jumuiya, tulipotoka na tunakoelekea. Katika Mkutano huu wamajumuiya watapata fursa ya:

·      Kusikia kutoka kwa kila kiongozi wa Jumuiya ni nini kila kiongozi alichokifanya tokea achaguliwe Oktoba 2013 mpaka sasa;

·      Kusikia jinsi ya Bodi na Kamati Kuu zinavyofanya kazi pamoja na ni nini “future” ya Jumuiya kwa ujumla;

·      Kupata taarifa ya mahesabu kutoka kwa Mweka Hazina;

·      Kupata Taarifa ya Katibu kuhusu Jumuiya tangu Mwaka Jana Oktoba mpaka sasa;

·      Kuuliza maswali na kutoa mapendekezo ya nini wanachotaka kifanyike katika kipindi kingine cha miezi sita ijayo.

 “please, save this date for our community meeting”. 
Ukipata taarifa hizi tunaomba umwambie mwenzako. Na tunawaomba wote mje kwa wingi tarehe 2 Agosti 2014 kwenye mkutano wa Jumuiya yetu.

Kutakuwepo na vinywaji na refreshments.

Asanteni, na kwa niaba ya viongozi wote,

Katibu,
Deogratius Mhella.
New York Tanzanian Community.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...