Waziri wa Biashara
Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed
Mazrui akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa maonyesho ya biashara ya Eid
El Fitri katika viwanja vya Maisara, wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya
Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), Sabetha Mwambenja na katikati
ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade Bi. Anna Bulondo.
Waziri wa Biashara
Viwanda na Masoko Nassor Ahmed Mazrui akiangalia bidhaa za wajasiriamali kwenye
maonyesho ya Biashara ya Eid El Fitri yanayofanyika katika viwanja vya Maisara,
pamoja nae katika picha kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade Bi.
Anna Bulondo, na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Thawabay Kisasi.
Waziri wa Biashara
Viwanda na Masoko wa Zanzibar Nassor Mazrui akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti
wa Bodi ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), Sabetha
Mwambenja wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbali mbali wa serikali na
TanTrade punde baada ya kufungua Maonesho ya Eid El Fitri visiwani humo. (Picha: Maelezo Zanzibar) .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...