Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana kutoka
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Bw. James Kajugusi akisisitiza
jambo wakati akiwahamasisha vijana wa Mchinga kujiunga katika vikundi vya
uzalishaji mali ili kuunda SACCOS ya vijana. Kulia ni Afisa Tarafa ya Mchinga,
Bi.Hadija Mringwa. (Picha
zote na Concilia Niyibitanga,Kitengo cha
Mawasiliano Serikalini,Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo)
Afisa Kata wa Kata ya Mchinga, Bi. Sharifa
Mkwango, akisisitiza jambo kuhusu vijana kujiunga katika vikundi vya
uzalizashaji mali.
Vijana wa Kata ya Mchinga, Lindi Vijijini wakifuatilia kwa makini maelekezo ya Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Bw. James Kajugusi (hayupo pichani) wakati akiwaelekeza namna ya kuunda vikundi na kupata mikopo kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Vijana mwishoni mwa wiki.
============ ======== =========
Serikali imewataka
vijana Mchinga kushiriki katika shughuli za maendeleo ili kujiinua kiuchimi na
kuleta maendeleo ya taifa kwa ujumla. Wito huo umetolewa
mwishoni mwa wiki na Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana, Bw. James
Kajugusi alipokuwa anaongea na Vijana wa Halmashauri ya Lindi Vijijini Kata ya
Mchinga jana kuhusu masuala ya maendeleo
ya Vijana.Bw. Kajugusi
amewaeleza vijana umuhimu wa kujiunga katika vikundi vya uzalishaji mali ili kuunganisha nguvu za kimtaji na kufikiri
kwa pamoja namna ya kuboresha maisha yao ya kila siku.
Vijana wanapokuwa
katika vikundi ni rahisi sana kutambulika nani yuko wapi anafanya nini na anahitaji
nini hivyo kuirahisishia Serikali kuwasadia. Amesema Bw. Kajugusi.
Amesema kuwa kijana
wa sasa anatakiwa kujitambua na kujua kuwa yeye ndiyo tegemeo la taifa hivyo
kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo yeye mwenyewe na taifa kwa
ujumla.
Changamoto kubwa ya
vijana ni kutojitambua hivyo kufikiri kwamba wanahitaji mitaji kwanza wakati
bado hawana hata wazo la kuwekeza na mtaji huo. Amesema Bw. Kajugusi. Amesema kuwa ni
muhimu vijana hao wakajiunga katika vikundi vya uzalishaji mali ili waweze kuunda
SACCOS yao kwa ajili ya kupata fedha ya mkopo kutoka katika Mfuko wa Maendeleo
ya Vijana ili kukuza mtaji na kuzalisha mali kwa ajili ya maendeleo endelevu.
Bw. Kajugusi amewaeleza
kuwa kupitia SACCOS ya vijana wataweza kupatiwa mikopo yenye riba nafuu ya
asilimia 10 ya mkopo ambapo asilimia 5 ya riba hiyo inabaki kwenye SACCOS
husika, asilimia 2 inabaki Halmashauri na asilimia 3 inarudi mfuko wa Maendeleo
ya Vijana ili kuutunisha na kuwawezesha vijana wengine kukopa. Aidha, amewataka
vijana kujali afya zao hususan kuepuka matumizi ya dawa za kulevya kwani
yanaharibu akili na viungo vya mwili hivyo kuathiri kiwango cha kufikiri na
kuathiri utendaji kazi na uzalishaji wa kijana.
Halikadhalika,
amewataka kujikinga na magonjwa ya zinaa na mimba za utotoni ili kushiriki
kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya jamii. Naye Afisa Tarafa ya
Mchinga, Bi. Hadija Mringwa aliwataka vijana wa Kata hiyo kuhakikisha kuwa
wanakamilisha zoezi la kujiunga katika vikundi na kuanzisha SACCOS mapema
iwezekanavyo ili waweze kufaidi fursa ya mkopo kutoka katika Mfuko wa Maendeleo
ya Vijana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...