Na Rose Masaka na Lorietha Laurence-MAELEZO 

TANZANIA ni miongoni mwa Nchi ambazo zimeweza kupunguza maambuzi ya ugonjwa wa Ukimwi kwa asilimia 33.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. William Lukuvi wakati akiwaeleza waandishi wa habari kuhusu Mkutano wa 20 wa Kimataifa wa Ukimwi Duniani uliofanyika Melbourne nchini Australia Julai mwaka huu.

Amesema kuwa hatua hiyo imefikiwa baada ya Serikali kuanza zoezi la kuzuia maambukizi kutoka kwa mama mjamzito kwenda kwa mtoto,  na tohari kwa wanaume hasa kwa jamii iliyokuwa haifanyi hivyo.

“Tohari zinaonyesha kwa wanaume inapunguza maambukizi kwa asilimia 60 na wanawake asilimia 44. Tiba ya UKIMWI kwa mama mwenye virusi vya UKIMWI inapunguza maambukizi mapya kwa mtoto kwa asilimia 97 na tiba kwa watu wazima wa kawaida inapunguza maambukizi mapya kwa asilimia 96,” amesema Lukuvi

Naye Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania Dkt. Fatma Mrisho amesema kuwa sababu zinazochangia maambukizi mapya ni pamoja na baadhi ya mila desturi potofu za kitanzania ,ikiwemo ndoa za utotoni, kurithi wajane, wanaume kuwa na wanawake wengi na kuogopa kupima afya.

Mkutano huo ulikuwa na kauli mbiu iliyosema “Ongeza hatua katika juhudi zote za kuthibiti Ukimwi” ulisisitiza mapambano dhidi ya Ukimwi yanahitaji njia mbalimbali ikiwemo ushiriki wa wadau na umuhimu wa kutenga fedha kwa ajili ya shughuli za Ukimwi kutoka vyanzo vya ndani ya nchi na taasisi.

Mkutano huo ulihudhuriwa na wajumbe 11,200 kutoka katika nchi 146 ikiwemo Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Wananchi waendelee kuhamasishwa ili maambukizi yapungue zaidi.

    ReplyDelete
  2. wanafiki wakubwa kuna wataalam wa kiatanzania ambao wamegundua tiba ya ukimwi wamekuleteeni ugunduzi wao hamuwapi support kwa sababu haina tija na nyinyi isipokuwa siasa za kushibisha vitambi vyenu.
    hamna hata haya.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...