Naibu waziri maji Amos Makalla leo ameongoza waumini wa kanisa kkkt dayosisi ya mashariki , viongozi wa majimbo na sharika zake katika harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa shule ya Elbeneza itakayokuwa kwa ajili ya shule ya msingi na sekondari.
Katika harambee hiyo fedha sh 124m zilipatikana kati ya hizo fedha taslimu sh 57m zilipatikana na 67m ikiwa ni ahadi. lengo la harambee ni kupata sh 120m kukamilisha majengo muhimu kuwezesha shule hiyo kufunguliwa januari mwakani.
Makalla alimpongeza askofu mameo, wachungaji na waumini kwa michango yao kufanikisha ujenzi
Aidha alilipongeza kanisa kwa uumuzi wa kujenga shule imeonyesha namba kanisa lilivyo tayari kushirikiana na serikali na amewahaidi kuzitafutia changamoto mbalimbali walizompatia kuziwasilisha serikalini.
Naibu Waziri Maji,Mh. Amos Makalla akitoa neno kwa ajili ya harambee ya kanisa la kkkt Bungo -Morogoro.
Naibu Waziri Maji,Mh. Amos Makalla akishiriki ibada ya harambee kanisa la kkkt Bungo-morogoro.
Naibu Waziri Maji,Mh. Amos Makalla akipata mkono wa baraka kutoka kwa baba askofu wa dayosisi ya mashariki baada ya harambee kanisa la Bungo- morogoro.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...