Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi Juliana Yassoda (Katikati) akiongea na Wanahabari (Hawapo pichani) kuhusu makocha wa Timu ya Barcelona kutoka nchini Hispania ambao wako nchini kwa ajili ya mafunzo ya makocha wa Tanzania yatakayofanyika kwa muda wa siku mbili.Wengine picha toka kulia ni Balozi wa Spain nchini Mh. Luis Manuel Ceuesta Civis, Mkurugenzi wa Masoko wa TBL,Kushila Thomas,Kocha Isaac Oriol Guerrero Hernandes,Kocha Daniel Bigas Alsina.mafunzo hayo yanatolewa kwa ushirikiano na Kampuni ya  Bia Tanzania (TBL).
Balozi wa Hispania nchini Tanzania Mh. Luis Manuel Ceuesta Civis (Kulia) akiongea na Makocha kutoka Timu ya Barcelona ya nchini Hispania katika mkutano wa Wanahabari uliofanyika jijini Dar es Salaam jana (leo), makocha hao wapo nchini kwa ajili ya kutoa mafunzo ya siku mbili kwa makocha wazalendo, wa kwanza kushoto ni Kocha Daniel Bigas Alsina na katikati ni Kocha Isaac Oriol Guerrero Hernandes
Kocha Isaac Oriol Guerrero Hernandes kutoka timu ya Barcelona ya nchini Hispania (katikati) akitoa maelezo kwa wanahabari (hawapo pichani) kuhusu mafunzo ya siku mbili watakayotoa kwa makocha 30 wakizalendo.kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Bi. Juliana Yassoda na wa kwanza kushoto ni kocha Kocha Daniel Bigas Alsina.
Makocha wa Kizalendo 30 ambao wanatarajiwa kupewa mafunzo ya siku mbili kutoka kwa makocha wa Barcelona wakiwa katika picha ya pamoja Picha zote na Benjamin Sawe kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WHVUM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hivi sasa Barcelona na Spain mpira wao umeshajulika hivyo timu zitakazo fuata mfumo wa Barcelona, Brazil na Spain hazitafika mbali. Mfumo mzuri wa kuigwa sasa ni mfumo wa Real Madrid, Atletico Madrid, Ujerumani na Argentina.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...