MACHINE HII NA VIFAA VYAKE ILIIBIWA NCHINI TANZANIA NA KUUZWA NCHINI ZAMBIA MJINI LUSAKA. BAADA YA JITIHADA YA POLISI WA TANZANIA, POLISI WA KIMATAIFA NA POLISI WA ZAMBIA MACHINE ILIPATIKANA MWAKA 2013 LUSAKA IKIWA INATUMIKA NA WATU WALIYOINUNUA.


MHE BALOZI GRACE MUJUMA AKIMKABIDHI MACHINE DR. NICOLAUS MBILINYI MGANGA MKUU WA WILAYA (DMO)  YA MOMBA ILIYOKUWA IMEIBIWA MWAKA 2012.  KUTOKA KUSHOTO NI DEREVA ALIYEKUJA KUCHUKUWA MACHINE, DR LAWRENCE MWAMPASHI (DISTRICT AIDS CONTROL COORDINATOR) MHE. BALOZI GRACE MUJUMA, DR. NICOLAUS MBILINYI NA MTAALAM WA MACHINE HIYO AMBAYE ALITHIBITISHA KUWA MACHINE NDIYO YENYEWE AKIWA NA AFISA UBALOZI Bw.  RICHARD LUPEMBE AMBAYE HAYUPO PICHANI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Sasa, kweli kabisa mtu anaiba mashine ya kuhesabu CD4 akaifanyie nini au ndio anaipeleka kwenye hosptili yake binafsi. Kha! Iba nyingine tuwege na aibu jamani!

    ReplyDelete
  2. unafikiri mwizi ana akili msomaji mwenzangu. akija nyumbani kwako akakosa alichopanga kukuibia au kitu chochote cha thamani atakuibia hata kijiko. na usilogwe ukaacha kiporo chako cha wali na kisamvu chote atafagia kalaghabao. sijui huwa wanakuwa wamevuta bangi zinawapeleka msobe msobe na kuwasukuma kufanya vitu vya ajabu

    ReplyDelete
  3. Mambo gani haya ya kuiba mashine za hospitali..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...