Rais Kikwete, Waiziri wa Ujenzi Dkt.Magufuli, Naibu Waziri wa Maji Amos Makalla, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Musa Iyombe, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Joel Bendera, M/Kiti Kamati ya Miundombinu Profesa Kapuya, M/kiti Bodi Mfuko wa Barabara Dr.Wanyancha, M/kiti Bodi ya Makandarasi Consolata Ngimbwa, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mhandisi Mfugale na Wakandarasi wa mradi wa Magole - Turiani.
Nyumba za Makandarasi zitakazokabidhiwa kwa wananchi wa Wilaya ya Mvomero baada ya mradi kuisha.

Rais Jakaya Kikwete amemshuhudia Waziri wake Dkt.Magufuli akiitwa Jembe Jembe! na wananchi wa Gairo kutokana na utendaji kazi wake, hayo yametokea Kata ya Gairo Wilayani Gairo kwenye Mkutano wa hadhara.

Rais Kikwete yupo Morogoro katika ziara ya siku tano akikagua miradi ya maendeleo, awali aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya Magole - Turiani yenye urefu wa kilomita 48.6, inayogharimiwa na Serikali kwa shilingi bilioni 41.891 kule Mvomero na baadae akaendelea na ziara Wilayani Gairo. Ilifika kipindi Dkt.Magufuli aliitwa katika jukwaa kwa ajili ya kusalimia na kutoa neno ndipo wananchi walishangilia kwa nguvu huku wakiita Jembe Jembe!

Mara kwa mara Dkt.Magufuli amekuwa akiitwa Jembe kutokana na uchapaji kazi wake tangu awe Waziri miaka ya 1995. Hilo pia limeshuhudiwa wakati Rais Kikwete alipomsifu yeye (Dkt.Magufuli) pamoja na timu yake kwa uchapaji kazi katika wizara ya ujenzi.

Katika hatua nyingine Waziri wa Ujenzi ameruhusu kuzikabidhi nyumba za Makandarasi kwa wananchi wa Wilaya ya Mvomero pindi mradi utakapoisha ili zitumike kwa shughuli za maendeleo ya wanamvomero.

1995 -2005: Rais Mstaafu B.Mkapa alimpachika Dkt.Magufuli jina la askari wa mwamvuli kutokana na utendaji kazi wake mzuri

2005 - Todate: Wananchi wamempachika jina la Jembe! Ikiwa ni pamoja na Rais Kikwete kumsifia kwa uchapakazi wake!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...