SHIRIKA la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) ni Shirika la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar lililoanzishwa mwaka 1968 kwa madhumuni ya kununua na kuuza mazao ya wakulima kama vile karafuu, mbata, makonyo, pilipili hoho, makombe na mwani.
.jpg)
Visiwa vya Zanzibar ni visiwa vinavyosifika kwa uzalishaji wa zao la karafuu bora ambalo pia katika miaka mingi ya nyuma, vilitajika kwa uzalishaji wa kiwango cha juu cha karafuu duniani.
Wananchi wengi wakati huo walikuwa wakizithamini mno karafuu kutokana na umuhimu wake wa kuwapatia kipato, lakini, pia kama zao tegemezi la uchumi wa Zanzibar katika kupata fedha za kigeni kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wake.
Akizungumza na Zanzibar Leo katika mahojiano maalum ya mafanikio ya Shirika la Biashara la Taifa (ZSTC), Naibu Mkurugenzi Muendeshaji wa Shirika hilo, Jongo Suleiman Jongo, alisema,
ZSTC imepitia katika hatua mbalimbali za mafanikio na changamoto tokea lilipoanzishwa mwaka 1968.
.jpg)
Alisema, katika miaka ya 1980-90, Shirika la ZSTC pamoja na kuwa lilikua likiendeleza majukumu hayo, lakini, pia Serikali kwa nia safi ilitoa nafasi kwa wananchi wake wenye uwezo wa kulima na kusafirisha mazao ya mbata, pilipili hoho, makombe na mwani kufanya hivyo ili kuongezea kipato chao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...