Meneja
wa Kitengo cha Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kulia),
akikabidhi vitabu vya masomo ya sayansi vyenye thamani ya shilingi
milioni 4.5/-, kupitia Mradi wa ‘Airtel Shule Yetu’ kwa Mwakilishi wa
Afisa Elimu ya Sekondari Manispaa ya Temeke, Yasintha Kayoza kwa niaba
ya shule tatu za sekondari za Mbagala, Mvuti na Kambangwa katika hafla
iliyofanyika kwenye Shule ya Sekondari ya Mbagala jijini Dar es Salaam
jana. Kushoto ni Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mbagala, Mwalimu Marcelina Kimario.
Meneja wa Kitengo cha Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (mwenye
miwani), akiangalia moja ya vitabu vya masomo ya sayansi baada ya
kuvikabidhi vitabu vyenye thamani ya milioni 4.5/-, kupitia Mradi wa
‘Airtel Shule Yetu’ kwa shule tatu za sekondari za Mbagala, Mvuti na
Kambangwa katika hafla iliyofanyika kwenye Shule ya Sekondari ya Mbagala jijini Dar es Salaam jana.
Meneja
wa Kitengo cha Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kulia),
akikabidhi vitabu vya masomo ya sayansi vyenye thamani ya milioni 1.5/-,
kupitia Mradi wa ‘Airtel Shule Yetu’ kwa Mkuu wa Shule ya Sekondari ya
Mbagala, Mwalimu Marcelina Kimario katika hafla iliyofanyika shuleni
hapo jijini Dar es Salaam jana. Sekondari nyingine zilizokabidhiwa
vitabu hivyo ni pamoja na Mvuti na Kambangwa. Kushoto ni Mwakilishi wa
Shule ya Sekondari Kambangwa, Mwalimu Sueiba
Mfinanga.
Mfinanga.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mbagala wakifurahia vitabu vya
masomo ya sayansi, baada ya Kampuni ya Airtel kupitia Mradi wake wa
‘Shule Yetu’ kukabidhi vitabu hivyo vyenye thamani ya milioni 4.5/- kwa
shule tatu za sekondari za Mbagala, Mvuti na Kambangwa katika hafla
iliyofanyika shuleni hapo jijini Dar es Salaam jana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...