Meneja Usimamizi, Undeshaji na Mazingira toka Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaama (DAWASA), Bi.Modesta Mushi akiwaneosha Wajumbe wa Bodi ya Wakurungenzi wa mamlaka hiyo ramani ya Ujenzi wa Mradi wa Bwawa la Kidunda lenye ujazo wa Mita milioni 190, Agosti 29, 2014 wakati wa ziara ya Bodi hiyo katika eneo la Mradi Mkoani Morogoro.
Mkuu wa Timu ya Ulipaji fidia kwa Wakazi walio katika Eneo la Mradi, Mhandisi. John Kirecha akitoa maelezo kwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurungenzi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA), kuhusiana kukamilika kwa taratibu za ulipaji fidia kwa wakazi waliopisha ujenzi wa mradi wa bwawa la Kidunda litakaloweza kutoa huduma kwa mikoa ya Dar es salaam, Pwani na Morogoro, wakati wa Ziara ya hiyo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA), Bw. Archard Mtalemwa akisisitiza jambo.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurungenzi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA), Alhaji Said El-Maamry (kulia), akimuuliza swali Mhandisi. John Kirecha kuhusiana fidia kwa Wakazi walio katika Eneo la Mradi huo, likiwemo kuhakikisha taratibu hizo haziathiri maendeleo ya ujenzi wa huo.
Mkuu wa Timu ya Ulipaji fidia kwa Wakazi walio katika Eneo la Mradi, Mhandisi. John Kirecha akitoa maelezo kuhusiana na taratibu za ulipaji fidia kwa wananchi hao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...