Washiriki wa maonesho, wananchi mbalimbali wakiwa katika maandamano ya kuadhimisha
Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani iliyozinduliwa katika Kiwanja cha Mpira wa Amri
Abeid jijini Arusha leo. Mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mrongo
aliyazindua maonesho hayo huku akiwataka madereva nchini wawe makini kwa kufuatia sheria
za barabarani ili kuepuka ajali. Kauli mbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu ni “Maamuzi yako
Barabarani Hatma Yetu-Fikiri Kwanza”.
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mrongo akitoa hotuba ya ufunguzi wa
Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani alioizindua Kitaifa jijini Arusha leo.
Kauli mbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu ni “Maamuzi yako Barabarani Hatma Yetu-Fikiri
Kwanza”. Katika hotuba yake, Mrongo aliwataka viongozi wa usalama barabarani kuhakikisha
kuwa adhabu dhidi ya madereva wazembe nchini inaongezeka ili wawe na woga wa kufanya
makosa barabarani.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima (kushoto) akimpa zawadi ya
ngao Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mrongo baada ya mgeni rasmi huyo
kuyafungua Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani ambapo kwa mwaka huu
maadhimisho hayo kitaifa yanafanya jijini Arusha. Kauli mbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu
ni “Maamuzi yako Barabarani Hatma Yetu-Fikiri Kwanza”.
Waendesha pikipiki (bodaboda) pia walishiriki kikamilifu katika uzinduzi wa maonesho hayo
yaliyofanyika katika Kiwanja cha Mpira cha Amri Abeid, jijini Arusha leo. Kauli mbiu ya
Maadhimisho ya mwaka huu ni “Maamuzi yako Barabarani Hatma Yetu-Fikiri Kwanza”.
Trafiki Makao Makuu jijini Dar es salaam, Mkaguzi Msaidizi, Yohana Mjema (kulia), akitoa
maelezo kwa mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mrongo (watatu kushoto), namna
ajali barabarani zinavyoweza kuepukika endapo watumiaji barabara watakuwa waangalifu kwa
kufuata sheria za barabarani. Mkuu wa Mkoa aliyazindua maonesho hayo ya Wiki ya Nenda kwa
Usalama Barabarani katika Kiwanja cha Mpira Amri Abeid jijini Arusha leo. Wapili kushoto ni
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima, na kushoto ni Mkuu wa Kikosi
cha Usalama Barabarani, Kamishna Msaidizi Mohamedi Mpinga.
Sajenti wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Damian Muheya (kulia) akiwaelimisha wananchi
wa jijini Arusha jinsi mtungi mdogo wa kuzimia moto unavyotumika wakati moto unapotokea.
Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani imezindulia leo na Mkuu wa Mkoa wa Arusha (Magesa
Mrongo katika Kiwanja cha Mpira cha Amri Abeid jijini humo. Kauli mbiu ya Maadhimisho
ya mwaka huu ni “Maamuzi yako Barabarani Hatma Yetu-Fikiri Kwanza”.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mrongo (katikati waliokaa), Naibu Waziri wa Mambo ya
Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima (wanne kutoka kushoto-waliokaa) wakiwa na wajumbe wa
usalama barabarani katika picha ya pamoja baada ya uzinduzi wa maonesho ya Wiki ya Nenda
kwa Usalama Barabarani ambayo Kitaifa mwaka huu yanafanyika jiijini Arusha leo. Kauli mbiu
ya Maadhimisho ya mwaka huu ni “Maamuzi yako Barabarani Hatma Yetu-Fikiri Kwanza”.
Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Wiki ya nenda usalama ituhamasishe kufuata sheria za barabarani mwaka mzima.
ReplyDeleteNimeangalia picha zenye mabati hapo juu, naona kwa ajili ya kupendezesha miji yetu yanahitaji kubadilishwa. Tunapenda sana kuzungumza kuhusu kutengeneza ajira lakini tunasahau kwamba ajira hizi zitaongezeka tutakapo nunua bidhaa zinazotengenezwa na viwanda vyetu wakati zinapohitajika.
Polisi inatisha !
ReplyDeleteSi mchezo !
Ohhh Chadema tunaandamana nchi nzima ile juzi ilikuwa ni rasha rasha tu, sasa je ni vipi Makao Makuu yenu Arusha (Dodoma yenu) leo Maandamano ni ya Wiki ya Usalama Barabarani?
Ajali nyingi ni uzembe wa mamlaka usika kutochukulia sheria madereva wazembe na walevi. Polisi wanawajua fika madereva wote wazembe pamoja name mabasi mabovu , lkn rushwa inanuka. Siku wakiamua kufanya kazi ajali sitapungua mno. Askari Saba mpaka kumi wanakaa sehemu moja wakati maeneo yapo kibao watu wanavunja sheria hasa kwenye traffic light, pikipiki zimekuwa kama taa haziwahusu pamoja na daladala. Hakuna anayechukuliwa sheria mambo ni yaleyalena akishikwa wanamalizana. Sasa lini nchi itaongozwa kikisheria? Hakuna miujiza ya kuzuia ajali mpaka polisi na idara zake zote zikubali kuna tatizo la uongozi otherwise don't waste our time na hizi sherehe zisizokuwa na solutions.
ReplyDeletetupatieni takwimu?
ReplyDelete