Hadi kufikia sasa PFT imefanikiwa kuunda jumla ya vikundi
150 vyenye wanachama 3,865 , wanawake wakiwa 3469 na wanaume 396, wanachama hao
wamewekeza jumla ya sh. 1,443,806,510 kupitia mpango wa ununuzi wa hisa za kila
wiki.
Katika risala yao wanachama hao wapya wa kutoka taasisi ya PFT walisema “Bodi ya wakurugenzi ya PFT na wanachama wote wa vicoba vinavyoratibiwa na Poverty Fighting Tanzania wameiomba NSSF kupitia Saccos Scheme iwasaidie kupunguza tatizo la mitaji midogo kwa wanachama wa vicoba kwa kuwapatia mkopo ambao kwa nidhamu waliyonayo wanachama wa vicoba wataweza kurudisha kwa wakati kwa mujibu wa makubaliano yatakayofikiwa, ilisema sehemu ya risala hiyo.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa NSSF. Dk. Ramadhani Dau akijibu Risala yao alihaidi kuwakopesha wana PFT kupitia NSSF SACCOS Scheme shilingi za kitanzania bilioni 1.5.
Semina endelevu za FURSA zinaendelea nchi nzima kwa udhamini wa NSSF ili kuweza kuwafikia wanachama,wa Hiari zaidi kama hawa wa PFT.
Semina hizi zinatarajiwa kusaidia kutoa elimu kwa Umma na uandikishaji wa Wanachama kwa mpango wa NSSF Hiari Scheme kote nchini ili kujikwamua na umaskini na maradhi kwa kupitia mafao ya NSSF na Pensheni.
Mbunge
wa Temeke, Abbas Mtemvu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi
ya Poverty Fighting Tanzania (PFT), akimkaribisha Mkurugenzi Mkuu wa
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk. Ramadhan Dau mara baada
ya kuwasili katika ukumbi wa mikutano wa PTA jijini Dar es Salaam
ambapo alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya kukabidhi kadi kwa wanachama
wapya wa Vicoba kutoka vikundi 150 vinavyoratibiwa na taasisi ya Poverty
Fighting Tanzania.
Katika risala yao wanachama hao wapya wa kutoka taasisi ya PFT walisema “Bodi ya wakurugenzi ya PFT na wanachama wote wa vicoba vinavyoratibiwa na Poverty Fighting Tanzania wameiomba NSSF kupitia Saccos Scheme iwasaidie kupunguza tatizo la mitaji midogo kwa wanachama wa vicoba kwa kuwapatia mkopo ambao kwa nidhamu waliyonayo wanachama wa vicoba wataweza kurudisha kwa wakati kwa mujibu wa makubaliano yatakayofikiwa, ilisema sehemu ya risala hiyo.
"Imani yetu ni kwamba NSSF
itaendelea kushirikiana nasi na kutusaidia kupata mafao yaliyoainishwa ambayo mwanachama
anastahili".
Poverty Fighting Tanzania imeunga mkono kwa vitendo kampeni
ya kitaifa ambayo NSSF ni wadau wakubwa wa “Kamata Fursa Twende Zetu”
Nae Mkurugenzi Mkuu wa NSSF. Dk. Ramadhani Dau akijibu Risala yao alihaidi kuwakopesha wana PFT kupitia NSSF SACCOS Scheme shilingi za kitanzania bilioni 1.5.
Semina endelevu za FURSA zinaendelea nchi nzima kwa udhamini wa NSSF ili kuweza kuwafikia wanachama,wa Hiari zaidi kama hawa wa PFT.
Semina hizi zinatarajiwa kusaidia kutoa elimu kwa Umma na uandikishaji wa Wanachama kwa mpango wa NSSF Hiari Scheme kote nchini ili kujikwamua na umaskini na maradhi kwa kupitia mafao ya NSSF na Pensheni.
Naibu Meya wa Manispaa ya Temeke, Juma Mkenga (kushoto), akisalimiana na Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk. Ramadhan Dau
mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa mikutano wa PTA jijini Dar es
Salaam ambapo alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya kukabidhi kadi kwa
wanachama wapya 211 wa taasisi ya Poverty Fighting Tanzania.
Mgeni rasmi Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk. Ramadhan Dau akiwasili ukumbini huku akifuatana na Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Poverty Fighting Tanzania (PFT).
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...