Asasi Nne zisizo
za kiserikali zinazojishughulisha na kupambana na mabadiliko ya tabianchi
nchini ForumCC, CAN, YouthCAN na Oxfam Tanzania zimetoa tamko la pamoja kuhusiana
na Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi utakaofanyika huko
New York-Marekani tarehe 23/09/2014.
Katika tamko
hilo ambalo pia limewasilishwa kwa Waziri
wa
Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira, Dr. Eng. Binilith
Mahenge, mambo matano yamependekezwa kuzingatiwa
wakati wa mkutano huo ambao Rais wa Tanzania DK. Jakaya Kikwete pia atatoa
hotuba yake.
Mambo hayo ni
pamoja na kupunguza utoaji wa hewa ukaa (Emission Reduction), Misaada ya Fedha
za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi (Climate Finance), Kuongeza mapambano
ya mabadiliko ya tabianchi kwa vitendo, Matumizi ya teknolojia na Nishati
Mbadala na Kilimo.
Waziri
wa
Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira, Dr. Eng. Binilith
Mahenge(katikati) akiwa na Viongozi wa Forum CC, kutoka kulia ni Oscar
Munga, Mjumbe wa bodi ya wadhamini ya ForumCC, Vera Mugita, Afisa
Miradi, Fazal Issa na Adam Anthony.
Waziri
wa
Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira, Dr. Eng. Binilith
Mahenge wa kwanza kushoto akizungumza na Mjumbe wa bodi ya wadhamini ya ForumCC, Vera Mugita na Afisa
Miradi wa ForumCC Fazal Issa
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...