KLABU ya Topland ya Mkoa wa Kimichezo wa Kinondoni yenye makazi
Magomeni jijini Dar es Slaaam imefanikiwa kutetea ubingwa wa ke
wa fainali za mashindano ya Safari Pool Taifa yaliyomalizika mwishoni
mwa wiki Mkoani Kilimanjaro kwa kuifunga timu ya Anatory ya Mkoani
Morogoro 13-3.
Timu ya Topland kwa kutwaa ubingwa huo ilizawadiwa Kikombe,Medali
za dhahabu na pesa taslimu Shilingi 5,000 000/= wakati mshindi wa pili
Anatory ya Morogoro walizawadiwa pesa taslimu Shilingi 2,500 000/=
pamoja na medali za fedha.
Mshindi wa tatu katika fainali hizo ni timu ya Mashujaa kutoka Mkoa
wa kimichezo wa Ilala jijini Dar es Salaam ambao walizawadiwa
fedha taslimu Shilingi 1,250,000/= pamoja na medali za shaba wakati
washindi wanne ni timu ya Mboya ya Mkoani Kilimanjaro ambao ndio
walikuwa wenyeji wa Mashindano hayo kwa mwaka 2014 ambao
walizawadiwa pesa taslimu Shilingi 750,000/=.
Upande wa mchezaji mmoja mmoja Wanaume, Mussa Mkwega kutoka
klabu ya Anatory ya Mkoani Morogoro alitwaa ubingwa kwa kumfunga
Innocent Sammy kutoka Mkoa wa kimichezo wa Temeke 5-4 na hivyo
Mkwega kuzawadiwa fedha taslimu Shilingi 500,000/=,medali ya
dhahabu pamoja na ngao wakati Innocent Sammy kwa kuchukua nafasi
ya pili alizawadiwa fedha taslimu shilingi 250,000/= pamoja na medali
ya fedha.
Upande wa mchezaji mmoja mmoja wakina Dada, Neema Hamis kutoka
Mmkoa wa Tanga alitwaa ubingwa kwa kumfunga Sada Tulla kutoka
Shinyanga na hivyo kuzawadiwa pesa taslimu Shilingi 350,000/= pamoja
na medali ya Dhahabu wakati Sada Tullah yeye kwa kukamata nafasi ya
pili alizawadiwa pesa taslimu Shilingi 200,000/=.
Akikabidhi zawadi hizo Naibu Waziri wa Habari, Vijana,Utamaduni na
Michezo, Juma Nkamia aliipongeza Kampuni ya Bia Tanzania kupitia
bia yake ya afari Lager kwa kudhamini mashindano ya Pool Taifa na
alliwaomba waendelee kufadhili kwani mpaka sasa ni mchezo pekee
ulioiletea sifa Nchi kupia fainali za Afrika ambapo Mtanzania Patrick
Nyangusi anashikilia Ubingwa wa Afrika.
Nkamia aliwataka pia Chama cha Pool Taifa(TAPA) kutumia vyema fursa
ya TBL kwa manufaa ya kuendeleza mchezo huo nchini na Kimataifa na
kwa jinsi hiyo aliwapa siku 60 wawe wameshafanya uchaguzi na kupata
viongozi wa kuchaguliwa kikatiba na wa muda tangu chama hicho
kianzishwa kama ilivyo sasa.
Mwisho Waziri Nkamia aliwatakia safari njema wanamichezo wote
kurejea majumbani salama na kuwaomba walichokipata kwa Safari
Lager kama zawadi wakakitumie vyema kwa maezndeleo yao.
Nahodha wa timu Topland ya Mkoa wa kimichezo wa Kinondoni, Patrick Nyangusi akishangilia na kikombe mara baada ya kuibuka mabingwa katika fainali za mashindano ya Safari Pool Taifa yaliyomalizika mwishoni mwa wiki Mkoani Kilimanjaro.
Baadhi ya wachezaji wa klabu ya Topland wa mkoa wa kimichezo wa Kinondoni wakishangilia na kikombe pamoja na pesa taslimu Shilingi 5,000 000/= mara baada ya kuibuka mabingwa katika fainali za mashindano ya Safari Pool Taifa yaliyomalizika mwishoni mwa wiki Mkoani Kilimanjaro.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...