Hassan Tofi mmoja wa washiriki wa Shindano la Dance 100% wa Kundi la Best Boys la Kigamboni jijini Dar es Salaam,akiwaongoza wenzake katika mazoezi yao yanayofanyika katika Viwanja vya Don Bosco Upanga ikiwa ni sehemu ya kujindaa na fainali ya shindano hilo litakalofanyika hivi karibuni. Shindano hilo limeandaliwa na EATV na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.

WADAU wa muziki nchini wamewapongeza waratibu wa shindano la Dance 100% ambalo limefikia hatua ya fainali, baada ya makundi matano kupenya nusu fainali, Jumamosi iliyopita.

Kivumbi hicho kilichoshindanisha makundi 10 yalipenya hatua ya robo fainali, Iliyofanyika Viwanja vya Don Bosco, jijini Dar es Salaam na kuvuta hisia za wengi kutokana na umahiri wa kila kundi.

“Nikiwa miongoni mwa watu waliojitokeza kushuhudia shindano hili, nimepata burudani kubwa na kujifunza mengi, vijana wameonyesha vipaji na uwezo wa kiwango cha hali ya juu,” alisema Ramadhan Malenge ‘Ramso.’

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...