
Na Benedict Liwenga, Maelezo-Dodoma.
Kanuni za Bunge Maalum hususani Kanuni ya 77 inawataka waandishi wa habari kuandika habari za Bunge Maalum kwa weledi mkubwa na kuzingatia maadili ya uandishi wa habari ili kujiepusha na uandishi wenye utashi na ushabiki wa kisiasa, msukumo binafsi, chuki ama uchochezi na wakati mwingine uongo wa makusudi.
Aidha, katika Kanuni hiyo hiyo ya 77(3) inatamka bayana ya kuwa “Katibu anaweza wakati wowote kuondoa ruhusa aliyotoa kwa mwakilishi wa Chombo chochote cha habari iwapo chombo hicho kitatoa taarifa yoyote kuhusu shughuli za Bunge Maalum ambayo kwa maoni ya Bunge Maalum inapotosha ukweli au vinginevyo inakiuka Kanuni, taratibu au haki za Bunge Maalum”.
Vyombo vya habari vina haki ya kupata habari ili viweze kuhabarisha umma juu ya mambo mbalimbali yanayoendelea nchini has katika Bunge Maalum la Katiba, lakini katika kufanya hivyo waandishi wa habari wanapaswa kutenganisha kati ya siasa na uandishi wa habari, hivyo wanapaswa kubainisha na kuainisha dhana ya uandishi wa habari za kibunge wenye tija kwa taifa ambayo ni weledi katika uandishi wa habari, uelewa kuhusu matarajio ya wananchi pamoja na uelewa juu ya dhima na dhamira ya Bunge katika taifa.
Uandishi wa habari ni vema usitumiwe kama njia ya kufikia malengo ya kisiasa ama mtu binafsi, makundi au chama na kitendo cha mwanasiasa kuvaa koti la uandishi wakati ni mwanasiasa kunajenga chuki, kunaharibu heshima ya uandishi wa habari na maisha ya waandishi.
Endapo siasa zitaingizwa katika uandishi wa habari basi kuna hatari ya kuilisha jamii yetu uongo. Mfano, kifungu cha 25 cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba kinavyotafsiriwa kisiasa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...