Habari Ankal Michuzi,
Bila shaka wewe ni bukheri wa afya. Nakupongeza kwa kazi adhimu ya kulihabarisha taifa. Basi na mimi bila kusita naomba kupitia kwenye globu hii maarufu ya jamii nipate kuwahabarisha watanzania wote wanaopenda maisha juu ya libeneke jipya la maakuli.
Nina furaha na shauku kubwa ya kuwaambia watanzania wenzangu kuwa tunawaletea libeneke jipya la Misosi – Ladha ya Maisha. 
Libeneke la http://www.misosi.co.tz/home ni maalumu kwa kupata habari za mapishi pamoja na kutafuta huduma za kijamii karibu nawe – mfano kujua sehemu za kula au maduka ya bidhaa za nyumbani karibu na ulipo.
Lengo kubwa la tovuti hii ya Misosi ni kuchangia na kubadilishana ujuzi kuhusu mambo ya maisha ya kila siku, hasa kuhusu afya ya familia. Tunaamini kila kitu kina jibu, na penye wengi hakukosi mafanikio, jumuika nasi kwenye misosi.co.tz ili tupate kupata ufumbuzi wa maisha kwa urahisi.
Ni wazi kuwa katika pilika zetu za maisha ya kila siku huwa tunakosa muda wa kupanga ratiba nzuri za kujua tunafurahiaje maisha baada ya kazi. Mama akiwa nyumbani au kazini anakuwa na kazi ngumu ya kupanga mipango kuhusu maakuli na afya ya familia. Hii si kazi rahisi hata kidogo.
Misosi imetambua kilio hicho na kutafuta njia mbadala ya kutatua tatizo na kuokoa muda wa mama kufanya maamuzi magumu ya nyumbani kwa kuweka uwanja mpana wa kuchagua kilicho bora na rahisi karibu yake. Kuzingatia hilo, mtandao wa Misosi unakidhi haja kwa kutoa majibu kwa maswali yote yanayohusu mapishi, afya, pamoja na mahitaji ya kila siku nyumbani kwa urahisi.
Misosi haishii kwa mama tu nyumbani, bali ni suluhisho kwa kila mmoja wetu – baba na watoto. Kwa kuhakikisha hili, angalia kama utajibu ‘Ndiyo’ kwenye Kipengele chochote kati ya hivi vifuatavyo:

1. Je unapenda kujifunza mapishi?

Misosi inatoa nafasi ya kujifunza mapishi au kupata mawazo juu ya nini cha kuandaa kirahisi nyumbani. Misosi.co.tz tunaweka maelekezo rahisi ya kuandaa vyakula vya aina mbali mbali. Kama unapenda kubadilisha ladha ya mapishi, au unapenda kujifunza kuhusu mambo mapya, basi misosi ndio nyumbani kwako. Ukitaka kusoma mapishi au habari za blog ya Misosi ni bure, na hakuna masharti yeyote, tembelea tu http://www.misosi.co.tz/home.

2. Je unapenda kuchangia ujuzi wako wa mapishi?

Je wewe una ujuzi wa kuwafunza wengine? Misosi inakukaribisha kuchangia mawazo yako. Kama unaopenda kuchangia ujuzi wa mapishi mbalimbali, misosi inakupa nafasi ya kuweza kutimiza hilo. Unachohitaji ni kujisajili bila gharama yeyote na kuweka mapishi yako. Kujisajili ni rahisi sana na inachukua dakika 2 tu. Kila kitu kimerahisishwa kuhakikisha unafanya vitu kwa ufanisi na haraka. Kujisajili sasa bofya hapa.

3. Je una biashara ya vyakula au bidhaa za nyumbani ?

Misosi inakutanisha watu wa kila aina, na hasa wale wanaopenda kujua bidhaa nzuri zinapatikana wapi. Sasa, kama una biashara na unahitaji kuwafikia wateja wako kirahisi, basi misosi ndio mkombozi wako. Misosi inakupa nafasi ya kusajili biashara yako bila gharama yeyote. Lengo likiwa kutoa taarifa sahihi za upatikanaji wa huduma karibu na walaji. Ukitaka kusajili biashara yako bofya hapa.

Kwanini ujisajili na Misosi.co.tz ?

Kujiunga na misosi hakuna gharama yeyote. Na hizi ndio faida utakazipata ukijisajili nasi:
·         Unakuwa na uhuru wa kuweka mapishi bila kikomo
·         Unakuwa na uhuru wa kuweka biashara yako BURE na kuwafikia wateja kwa urahisi!
·         Unaweza kuchangia mada tofauti kuhusiana na misosi
·         Unaweza kuweka biashara yako na kufuatilia maoni ya wateja wako
·         Unaweza kutangaza matukio kama sherehe au mikutano bure kupitia tovuti
·         Unaweza kuweka habari kuhusiana na chakula, afya au biashara yako bure.
·         Unakuwa mmoja wa jumuiya ya watu wenye fikra chanya kama zako. Unapata kusikia mawazo chanya toka kwa watu wenye mtazamo unaofanana na wako. Vilevile mawazo yako yanapata kuwafikia wale walengwa wako kwa urahisi zaidi na wakati muafaka.

Karibuni sana kwenye libeneke la misosi. Karibuni sana tujirambe na ladha ya maisha.
– Misosi Team

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...