Meneja Kiongozi wa
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mwanza, Bw. Hamis Faki (wa pili
kushoto) akitoa hotuba wakati wa kuhitimisha Mbio za Rock City Marathon
zilizofanyika jijini Mwanza Jana.
Katibu Mkuu wa Chama cha
Riadha nchini Suleiman Nyambui,akiwapa maelekezo wakimbiaji wa Km 21, kabla ya
mbio kuanza,kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Mratibu wa Mbio za Rock
City Marathon 2014 kutoka kampuni ya Capital Plus International Limited (CPI),
akizungumza na waandishi wa habari juu ya muitikio mkubwa ulionyeshwa katika
Mbio za mwaka huu zilizofanyika Jijini Mwanza Jana.
Mwanariadha
kutoka Mkoani Manyara Joseph Panga,akimaliza mbio za KM 21 kwenye
Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza jana,wakati wa mbio za Rock City
Marathon 2014, akifuatiwa na Sammy Nyokaye kutoka Kenya(kulia).
Wanariadha wakianza kukimbia mbio za km 21 kwenye Uwanja wa
CCM Kirumba jijini Mwanza jana,wakati wa mbio za Rock City
Marathon 2014.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...