Mkurugenzi kutoka wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa anaeshughulikia dawati la diaspora,Bi Rosemary Chambe Jairo akifungua rasmi mkutano wa Watanznia waishio nchini Botswana wakati walipokutana na Ujumbe kutoka Mfuko wa GEPF ulikuwa ukiitambulisha mpango wa GEPF DIASPORA SCHEME (GDS) nchini humo,hivi karibuni.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania waishio nchini Botswana,Bw Kisasi akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi.
Mkurugenzi wa Uendeshaji kutoka Mfuko wa GEPF,Bw Anselim Peter akiwasilisha mada kuhusu mpango wa GEPF Diaspora Scheme (GDS) na faida zake wanachama.
Meneja Masoko wa Mfuko wa GEPF,Bw. Aloyce Ntukamazina akisisitiza juu ya umuhimu wa watanzania waishio Botswana kuanza kujiwekea akiba kupitia mpango huo wa GEPF Diaspora Scheme (GDS).
Baadhi ya Watanzania waishio Botswana wakifuatilia kwa makini mada zilizowasilishwa na mfuko wa GEPF.
Bw Jimmy Joseph Mwambije Mtanzania aishie Botswana akijaza fomu na kujiunga rasmi na mpango huo wa GEPF Diaspora Scheme (GDS).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...