Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Mhe. DK. Mary Nagu akiangalia samani wakati wa sherehe fupi ya uwekaji  saini makubaliano kati ya Funiture Center DSM na Shirikisho la Mafundi Samani Tanzania (TAWOFE) katika ofisi za Furniture Center Dar es Salaam.
  
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Mhe. DK. Mary Nagu akishudui uwekaji saini makubaliano kati ya Funiture Center DSM na Shirikisho la Mafundi Samani Tanzania (TAWOFE) tarehe 29 Oktoba, 2014 katika ofisi za Furniture Center Dar es Salaam. Makubaliano hayo, ni kuimarisha ushirikiano kwa kuingia ubia na wazalishaji wakubwa kama Furniture Center ili kunufaika na uwezo wao mkubwa kwenye maeneo muhimu kama mitaji, masoko ya bidhaa, teknolojia na vifaa vya kisasa vinavyofaa kutengenezea samani hizo.
Mhe. Nangu alisema, “ushirikiano wa namna hii utaboresha ununuzi wa bidhaa zinazopatikana nchini kwa urahisi na kukuza soko letu pia huu ni uzalendo wa hali ya juu uliooneshwa katika kuwawezesha mafundi samani kuingia katika soko la Kimataifa, wakijiamini kwamba bidhaa zao zina ubora wa Kimataifa na kupongeza uongozi wa Funiture Center DSM kwa hatua walioichukua”.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...