Napenda kutoa shukrani kwa uongozi wa Michuzi blog {BLOG YA JAMII} kwakile ambacho nimeweza kukipata kutoka kwenu. Mimi ni kijana wa miaka 20 Niko Chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha {AJTC} nachukua diploma ya utangazaji wa radio na Tv 

Ni moja ya watu ambao nilikuwa nikipenda sana kazi za michuzi blog nakutamani siku moja kuwa kama yeye. Nashukuru   Mungu Ndoto zimetimia sasa natambulika Arusha nzima, na  Uongozi wa chuo unanitumia kama mfano wa kuigwa kwa wanafunzi wengine kwani ni moja ya mtu ninayemiliki website ya burudani na  marika yote wanaweza kutembelea.

Sina chakukulipa ila nashukuru kwa kuweza kufikisha malengo yangu ya kumiliki Website. Naomba Mungu akupe uzima  japo nami nije kupata nafasi ya kukushika mkono wamshukrani  kwa hatua hii ya kumiliki www.jimmcarter.com 
natumaini ipo siku nitapata nafasi yakuonana na uongozi wa michuzi blog nitoe shukrani zangu.
-------------------------------------
Kaka shukurani umeshazitoa na kwa kuonesha kwa vitendo kile ulichokuwa unaota ni shukrani tosha kwangu. Najisikia  mwingi wa furaha na fahari kwa hayo uyasemayo, na nimeguswa sana sana nayo. Ni wachache wanaweza kuwa kama wewe. Nami nakukuhakikishia ushirikiano endelevu kwani naona kabisa utakuwa kileleni muda si mrefu ujao. Ushauri wangu kwa sasa ni kuweka mambo ya nyumbani kwa asilimia japo 60% na mambo ya nje fanya asilimia 40%. Hapo utakuwa umewatendea haki Watanzania kwa asilimia 100%. Vinginevyo kaza buti endeleza LIBENEKE!

Muhidin Issa Michuzi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Huu ndio UTU
    Huu ndio UJASIRI
    Huu ndio USTAARABU
    Kukiri na hasa KUKIRI WAZI kuwa ni wapi ulipata nia, msaada na hata chachu ya kufanikiwa kuwa ulivyo sasa.

    Hongera Jim
    Ungana nasi kwa maelfu ambao tulianza kumsima na sasa tunajivunia kutimiza sehemu ya ndoto zetu kwa masaada wa waliotutangulia kama Kaka Issa

    ASANTENI NYOTE

    ReplyDelete
  2. Tanx dady asante sana sinachakukulipa bt naamini maombi yangu kwako nimalipo tosha dady ushauri wako nitaufanyia kazi na mabadiliko nitakupa ripoti nashukuru dady inatia moyo kuendelea kufanya hichi nilichokichagua

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...