Na  Mwene Said 



Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), limesema usumbufu wa kukatika kwa umeme uliojitokeza wiki moja iliyopita limetokana na usafi wa visima vya mafuta na kwamba hadi kufikia kesho hali itarudi kawa kawaida.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ukaguzi wa mtambo wa kuchuja umeme Tandika,  jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Bw.Felchesmi Mramba (pichani)  alisema usumbufu huo ulitokana na Kampuni ya Pan Afrika kufanya usafi kwenye visima vyake vya mafuta.
"Kutokana kufanyika usafi wa visima vya mafuta gesi ni ndogo na kwamba imeathiri maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam... hali hiyo itakwisha leo na kuanzia kesho Novemba Mosi hali ya umeme itakuwa ya kawaida na usumbufu kwa wateja wetu utaisha" alisema Mramba.
Mbali na usumbufu huo, Mramba alisema shirika lake lina mkakati mkubwa wa kuondoa kero ya umeme kwa wakazi wa Mbagala, Kurasini, Mkuranga, Kigamboni, Chamazi, Tuangoma, Kurasini na Mtoni Kijichi wanaopata hudumu kutoka kituo cha Ilala sasa watahamishiwa kituo cha Kipawa kupitia Tandika.
Akifafanua zaidi alisema kituo cha Kipawa kitapeleka umeme kituo cha Tandika ambacho kitachuja na kupatikana Mega Wati 12.5 zitakaboresha huduma kwa wakazi wa maeneo hayo.
"Hadi kufikia Aprili mwaka 2015 shirika litatoa huduma nzuri kwa wakazi wa Dar es Salaam na kero ya umeme itakuwa historia... "alisema Mkurugenzi huyo wakati akikagua ukarabati wa kituo cha kuchuja umeme kilichopo Tandika, Wilaya Temeke.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...