Kazi ya kutambua kaya maskini ambazo zitaingizwa kwenye Mpango wa kunusuru kaya maskini unaoratibiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii –TASAF – imeshika kasi katika maeneo kadhaa ya mikoa ya Simiyu,Mwanza,Shinyanga,Morogoro,Tanga na Pwani.

Zoezi hilo la kuzibaini kaya za walengwa wa Mpango huo katika mikoa hiyo limeanza baada ya kukamilika kwa warsha za kuwajengea uelewa wawezeshaji wa ngazi ya Halmashauri ambao wamefanya pia mafunzo kwa wadodosaji kwenye maeneo ya vijiji .

Baada ya kukamilika kwa zoezi la utambuzi wa kaya za walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya maskini  kwenye mikoa hiyo taratibu zaidi za kiutendaji zitafuata baada ya madodoso hayo kupelekwa makao makuu ya TASAF ,DSM zoezi litakalowezesha walengwa kulipwa fedha kwa njia ya uhawilishaji fedha (cash transfer).

Zifuatazo hapo chini ni picha mbalimbali za walengwa wa Mpango huo wakihojiwa kwa lengo la kuweka kumbukumbu zao kwenye madodoso katika vijiji kadhaa vya wilaya ya Maswa mkoani Simiyu.
Mmoja wa maafisa wa TASAF  Hamis kikwape aliyeketi mstari wa mbele akifuatilia kazi ya utambuzi wa kaya maskini katika moja ya walengwa wa mpango huo wilayani Maswa. kazi ya utambuzi wa kaya maskini inaendelea kwa kasi katika maeneo ya wilaya ya Maswa mkoani Simiyu.
Pichani ni baadhi ya Watoto wakiwa na furaha tupu baada ya kupata maelezo juu ya mpango wa kunusuru kaya maskini wilayani Maswa.
Baadhi ya walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya maskini wilayani Maswa wakiwa katika picha ya pamoja na mmoja wa maafisa wa TASAF,Hamis Kikwape (mwenye suti nyeusi aliyeketi).
Walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini wilayani Maswa wakipewa maelezo ya mpango kabla ya kuorodheshwa .
 Wadodosaji wa taarifa za walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini wilayani Maswa wakiendelea na kazi hiyo katika moja ya kaya za walengwa wa mpango huo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...