Mkurugenzi wa Airtel Huduma kwa Wateja,Bi.Adriana Lyamba akimkabidhi kombe Nahodha wa timu ya Simba ya UDOM kwa kuibuka washindi wa mashindano ya Airtel Uni 255,yaliyofanyika katika viwanja vya michezo ndani ya Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM),Mashindano hayo yalifanyika mwishoni mwa wiki mkoani Dodoma.
 Timu ya Simba ikishangilia mara baada ya kukabidhiwa kombe lao mara baada ya kuibuka kinara katika mashindano ya Soka ya Airtel 255.
 Aidha Aneth Mugha ambaye ni Meneja Masoko wa Airtel alikifafanua mbele ya Wanafunzi wa UDOM (hawapo pichani),namna vocha mpya ya Airtel Uni 255 inavyoweza kuwanufaisha katika suala zima la kuperuzi kwa gharama nafuu kuliko zote wakiwa chuoni hapo.Bi, Aneth alisema kuwa Airtel Uni 255 ni huduma maalum kwa vyuo vikuu inayomuwezesha mwanafunzi kupata huduma nafuu ya mawasiliano ikiwemo kupiga simu, sms, na intanet ili kwasaidia wanafunzi kutumia huduma hiyo kujiendeleza kimasomo.
 Baadhi ya Wanafunzi wakishuhudia burudani mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye jukwaa la Airtel Uni 255,baada ya mashindano ya Soka kumalizika na kumpata mshindi,Wasanii waliotoa burudani kwenye jukwaa hilo ni Roma,Ney wa Mitego pamoja na Vanessa Mdee a.k.a V-Money na burudani nyingine,ambapo wasanii chipukizi walishindana kughani na kuibuka na zawadi mbalimbali zikiwemo simu za mikononi,fulana na nyinginezo.
 Baadhi ya Wanafunzi wa chuo cha Dodoma (UDOM) wakiwa jukwaa wakijiunga na huduma maalum ya UN 255,ambayo imetolewa kwa ajili yao.Airtel Uni 255 ni huduma maalum kwa vyuo vikuu inayomuwezesha mwanafunzi kupata huduma nafuu ya mawasiliano ikiwemo kupiga simu, sms, na intanet ili kwasaidia wanafunzi kutumia huduma hiyo kujiendeleza kimasomo.

Aidha Aneth Mugha ambaye ni Meneja Masoko aliwatangazia Wanafunzi wa UDOM,namna vocha mpya ya Airtel Uni 255 inavyoweza kuwafaidisha kuperuzi kwa gharama nafuu kuliko zote wakiwa chuoni hapo.
 Baadhi ya Wanafunzi wa UDOM wakishangilia burudani iliyokuwa ikitolewa kweye jukwaa la burudani la Airtel Uni 255,ambapo wasanii mbalimbali walitumbuiza akiwemo Ney wa Mitego,Roma Mkatoliki pamoja na Vanessa Mdee a.k.a V-Money.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...