Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania -TRL unasikitika kuwatangazia kuwa kuanzia leo jioni saa
10 hakutakuwepo huduma ya usafiri wa treni ya Jiji maarufu kama ' treni ya Mwakyembe' hadi
siku Jumatatu Novermba 17, 2014 huduma itakaporejea kama kawaida.
Ufafanuzi wa sababu za kusitishwa huduma umeeleza kuwa kichwa kimojawapo ambacho
hutoa huduma kimepelekwa Karakana Kuu ya Morogoro kwa ajili ya ukarabati maalum na
kwamba kinatarajiwa kurejeshwa Dar es Salaam jioni ya siku ya Jumapili.Novemba 16, 2014
baada ya kukamilika zoezi hilo la ukarabati.
Huduma zitarejea tena siku ya Jumatatu saa 12:30 asubuhi kuanzia kama kawaida kituo cha
Ubungo Maziwa.
Atakayesoma taarifa hii amwarifu mwenzake!
Uongozi wa TRL unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza!
Imetolewa na Afisi ya Uhusiano ya TRL
kwa Niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TRL
Mhandisi Kipallo Amani Kisamfu.
Dar es Salaam,
Novemba 13, 2014
Mbona kichwa kimoja tu hakifai? kitafutwe kingine kama sio vingine ili usafiri huo uwe wa uhakika na daima. Hamuoni kama munapoteza pesa nyingi sana kusitisha siku zote hizo. Uongozi husika angalieni hilo.
ReplyDelete