Wakimbia mbio za Makasia Wanaume wakianza kukimbia wakati wa fainali za Mkoa wa Kagera zilizofanyika mkoani humo mwishoni mwa wiki ambapo kikosi cha Eliud Prosper kilifanikiwa kutwaa ubingwa wa Mkoa upande wa Wanaume.
Wakimbia mbio za Makasia Wanawake wakianza kukimbia wakati wa fainali za Mkoa wa Kagera zilizofanyika mkoani humo mwishoni mwa wiki ambapo kikosi cha Eliud Prosper kilifanikiwa kutwaa ubingwa wa Mkoa upande wa Wanawake.

KIKUNDI cha Wanaume wapiga kasia cha Eliud Prpsper Mkoani Kagera kimeibuka na ubingwa katika fainali za Mkoa za mashindano yambio za mitumbwi chini ya udhamini wa bia ya Balimi Extra Lager zijulikazo kama “Balimi Boat Race 2014” na hivyo kikundi hicho kuzawadiwa pesa taslimu Shilingi 900,000/= pamoja na kuwakilisha Mkoa wa Kagera kwenye fainali za Kanda zinazotarajiwa kufanyika Desemba 6 mwaka huu jijini Mwanza.

Nafasi ya pili ilichukuliwa na kikundi cha Zadock Ezekiel ambacho kilizawadiwa pesa taslimu Shilingi 600,000/= pamoja na kuwakilisha mkoa katika fainali za Kanda jijini Mwanza pia, wakati nafasi ya tatu ilichukuliwa na kikundi cha Eliakim Zadock ambacho kilizawadiwa pesa taslimu Shilingi 500,000/= na nafasi ya nne ilichukuliwa na kikundi cha Steven Nestor ambacho kilizawadiwa Shilingi 400,000/= Nafasi ya tano hadi ya tisa walipewa kifuta jasho cha pesa taslimu Shilingi 250,000/= kila kikundi ambavyo ni Laurent Laurian, Alex Andrew, Dalius Kiiza, Edwin John,Mwesiga Dan na Johnson John.

Upande wa Wanawake kikundi cha Khadija Ramadhan kilifanikiwa kutwaa ubingwa na hivyo kuzawadiwa pesa taslimu Shilingi 700,000/ = pamoja na nafasi ya kuwakilisha mkoa katika fainali za Kanda jijini Mwanza.Nafasi ya pili Wanawake ilichukuliwa na kikundi cha Salome Elnest ambao walizawadiwa Shilingi 600,000/=,washindi wa tatu ni kikundi cha Fredina Enerico ambao walizawadiwa Shilingi 400,000/= na nafasi ya nne ilichukuliwa na kikundi cha Agnes Matunga ambao walizawadiwa Shilingi 300,000/= na nafasi ya tano hadi ya kumi walizawadiwa kifuta jasho cha Shilingi 200,000/= kila kikundi ambavyo ni kikundi cha Halima Ahmad, Melesiana France, Anagrace Joseph, Paxdia Baitu na Zuhura Abdala.

Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi Meneja Matukio wa Kanda ya Ziwa TBL, Erick Mwayela alishukuru vikundi vyote vya Mkoa wa Kagera vilivyojitokeza kushiriki fainali hizo na kuwaomba waendelee na maandalizi vyema kwa fainali za Kanda zinazotarajiwa kufanyika Desemba 6, mwaka huu jijini Mwanza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...