Mkurugenzi
wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ephrahim
Kwesigabo, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo kuhusu Siku ya
Takwimu Afrika itakayo adhimishwa Dar es Salaam kesho. Kulia ni Mtakwimu Mkuu,
Adella Ndesengia.
Mkurugenzi
wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ephrahim
Kwesigabo, akisisitiza jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo jijini Dar es Salaam kuhusu
Siku ya Takwimu Afrika itakayo adhimishwa Dar es Salaam kesho.
Mkurugenzi
wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ephrahim
Kwesigabo, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) uliofanyika leo jijini
Dar es Salaam kuhusu Siku ya Takwimu Afrika itakayo adhimishwa Dar es Salaam
kesho. (PICHA NA VERONICA KAZIMOTO – MAELEZO).
Tanzania
itaungana na nchi nyingine barani Afrika katika kuadhimisha Siku ya Takwimu
Afrika ambayo itafanyika tarehe 27 Novemba, 2014 katika ukumbi wa mikutano
uliopo Jumba la Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza
leo na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii
Ephraim Kwesigabo wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu amesema lengo la kuadhimisha
siku hiyo ni kuongeza ufahamu kuhusu nafasi na mchango wa tasnia ya takwimu
katika kuleta maendeleo ya kiuchumi na
kijamii barani Afrika.Kwesigabo
amesema kuwa, Kaulimbiu ya Siku ya Takwimu Afrika kwa mwaka 2014 ni “Takwimu Huria kwa Uwajibikaji na Ushirikishwaji
wa Wadau wote”.
“Kaulimbiu
ya Siku ya Takwimu Afrika kwa mwaka huu imebeba ujumbe muafaka ambapo kwa kuwa
sasa maendeleo ya Afrika yanategemea takwimu huria katika kuongeza uwajibikaji
na ushirikishwaji katika kuandaa sera, kupanga na kutathmini mipango mbalimbali
ya maendeleo na kufanya maamuzi sahihi, amefafanua Kwesigabo”.
Takwimu huria ni takwimu na taarifa
zinazozalishwa kwa ubora na viwango kutokana na tafiti au taarifa za kiutawala
ambazo zinatolewa, kusambazwa na kutumiwa na mtu yeyote bila kikwazo chochote. Akielezea baadhi ya sifa za takwimu
huria Mkurugenzi Kwesigabo amesema ni pamoja na upatikanaji wake kwa urahisi
kulingana na mahitaji ya watumiaji, ziwe kamilifu kwa kutoa ujumbe sahihi na
unaoeleweka na ziwe katika mfumo
utakaomrahisishia mtumiaji kuzitumia
kulingana na mahitaji yake pasipo kizuizi chochote. Sifa nyingine za takwimu huria ni
kutokuwa na ubaguzi, zitolewe kwa wakati, na muundo wa uhifadhi wake uwe rahisi
ambao unaweza kusomeka katika programu mbalimbali za kompyuta.
Kwesigabo ameongeza kuwa Serikali
ya nchi yoyote inapokuwa na mfumo wa takwimu huria, huwezesha wananchi na wadau
wengine kupata taarifa na takwimu zinazozalishwa katika nchi hiyo bila kizuizi
chochote. Aidha, huongeza uwazi na ushirikishwaji wa wananchi katika uendeshaji
wa shughuli za Serikali.
Washiriki
mbalimbaliwa kutoka katika Wizara, Idara na Taasisi za Serikali, Wadau wa
Maendeleo, Vyuo vya Elimu ya Juu, Wanafunzi wa Shule za Sekondari pamoja na
Wadau wengine wa takwimu nchini wanatarajia kuhudhuria katika maadhimisho hayo. Maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika hufanyika tarehe 18 Novemba,
kila mwaka lakini kwa Tanzania maadhimisho hayo yatafanyika kesho tarehe 27
Novemba, 2014.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...