Afisa Masoko wa Silafrica bwana Alpesh Patel akikabidhi ufunguo wa gari aina ya Suzuki Carry jijini Dar leo kwa Mama Fatuma Wahenga kutoka kampuni ya FMJ Hardware,ambaye aliibuka mshindi wa pili kupitia promosheni iliyojulikana kwa jina la Uza na Ushinde.
 Afisa Masoko wa Silafrica bwana Alpesh Patel akizungumza kwa ufupi kuhusiana na promosheni yao iliyojulikana kwa jina la Uza na Ushinde na namna washindi wanavyopatikana.

 ========  =======  =======
Kampuni ya Silafrica Tanzania Ltd, inayoongoza kwa kutengeneza vifaa vya plastiki leo imemkabidhi gari aina ya SUZUKI CARRY mshindi wa pili wa shindano la Uza na Ushinde ambaye ni Mama Fatuma Wahenga kutoka F M J Hardware.

Akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya kukabidhi zawadi hiyo Jijini Dar es Salaam Afisa Masoko wa Silafrica bwana Alpesh Patel alisema promosheni iliwahusu mawakala wote wa bidhaa za SIMTANK kwa lengo la kuhamasisha ubunifu na kujituma miongo mwa mawakala hao.

“tunawashukuru mawakala wetu kwa juhudi zao na kujitoa katika kuuza bidhaa zetu, hivyo promosheni hii ililenga kuheshimu mchango wao, natumia fursa hii kuwashukuru mawakala wetu wote walioshiriki katika promosheni hii kwa kujitoa kwao na kufanya kazi kwa juhudi” Alisema Patel.

Bwana Alpesh pia alimshukuru Mama Wahenga kwa juhudi zake katika mauzo na kuwaomba mawakala wengine kuongeza bidii ili kujiweka katika nafsi ya zawadi kutoka SIMTANK siku zijazo.

Akipokea zawadi hiyo Mama Wahenga alishukuru SIMTANK kwa zawadi na juhudi zao katika kuboresha maisha ya mamilioni ya watanzania wanotumia huduma za maji safi na salama yaliyohifadhiwa katika tanki imara na salama SIMTANK kutoka Silafrica.

 “Kwanza nawashukuru, nitatumia gari hili kupandisha mauzo yangu kwa kuwafikia wateja wengi kwa wakati  hivyo  nitatimiza ndoto zangu za kuwa wakala kiongozi katika biashara ya kuuza SIMTANK.” Alisema, Mama Wahenga.



SIMTANK  walianza biashara yao miaka 20 iliyopita kwa lengo la kutoa huduma za kuhifadhi maji safi na salama katika vyombo imara salama na vyenye ubora katika nchi za Tanzania na Kenya, Kwa sasa SIMTANK ndiyo bidhaa inayoongoza na kuaminiwa katika soko kwa matumizi ya tekinolojia ya hali ya juu na matumizi ya malighafi imara. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...