Dkt Mary Nagu Waziri wa Uwekezaji na Uwezeshaji akiongea kwenye kongamano la uwekezaji kwa mikoa ya ukanda wa ziwa Tanganyika lililofanyika mjini sumbawanga mwishoni mwa wiki. hawapo pichani washiriki wa kongamano hilo
Washiriki wa kongamano la uwekezaji ambao ni wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi wakifuatilia kwa umakini mjadala wa kongamano hilo kwenye uwanja wa Nelsoni Mandela Mjini Sumbanga Mkoani Rukwa.

Na Kibada Kibada Rukwa.

Waziri wa Uwekezaji na uwezeshaji Dkt Mary Nagu amezishauri Taasisi za Kifedha hasa mabenki kupunguza riba inayotonzwa wakati wa kuomba mikopo ili kuwezesha wawekezaji Mwekezaji wa ndani na nje kukopa na kupata mitaji itakayomsaidia kuweza kuwekeza.

Alitoa ushauri huo mwishoni mwa wiki wakati wa Kongamano la Uwekezaji kwa Mikoa ya Ukanda wa Ziwa Tanganyika unaojumuisha mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma lililofanyika kwenye viwanja vya Nelsoni Mandela Mjini Sumbawanga Mkoani Rukwa.

Kongamano hilo lilihudhuriwa Viongozi mbalimbali, Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchiniWawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi, pamoja na wananchi wa mikoa ya ukanda wa ziwa Tanganyika hasa wakazi wa mjini Sumbawanga Mkoani Rukwa na lilifunguliwa na Makamu wa Rais Dkt Ghalib Bilal.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...